Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuwa mchangiaji wa mwisho kwenye Wizara hii ya Fedha. Kipekee nimshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya katika Taifa letu. vile vile, nimshukuru Dkt. Mwigulu, Waziri wetu wa Fedha pamoja na Naibu Waziri na timu yako yote kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kuifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nitachangia katika maeneo makubwa mawili. Eneo la kwanza nitachangia kuhusu mifumo ya ukusanyaji mapato hususani katika Serikali za Mitaa, lakini muda ukiniruhusu nitachangia kuhusu miradi mikubwa ya maendeleo na jinsi ya utoaji wa fedha kwenye hii miradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunatambua kwamba Serikali imefanya mageuzi makubwa sana katika ukusanyaji wa mapato hususani katika Serikali za mitaa. Huko nyuma tulikuwa na mfumo ambao ulikuwa unaitwa Local Government Revenue Collection Information System ambao ulikuwa unatumika kwa ajili ya kukusanya mapato. Hivi karibuni watu wa TAMISEMI wameboresha ule mfumo wamekuja na mfumo unaitwa TAUSI. Nataka nianze kujikita kwenye ule mfumo wa mwanzo ambao tunakwenda kuu–phase out iwe lesson kwa ajili ya jinsi gani tunakwenda ku–take off na ule mfumo wa TAUSI ambao tunakwenda kuanza nao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anajua kwamba katika mfumo wetu huu wa Local Government Revenue Collection Information System ulikuwa na changamoto nyingi sana. Changamoto ya kwanza ilikuwa ni suala la kutoa zile control number na hili nitatolea mfano kwenye ukusanyaji wa mapato. Naomba nitumie case study ya Manyoni. Katika Jimbo langu la Manyoni Mashariki tuna wakusanya mapato ambao wameajiriwa na halmashauri. Wale wakusanya mapato wanapokusanya ili waweze ku–bank wanapewa control number. Kuna changamoto kubwa sana kwenye huu mfumo wa kukusanya mapato hususani kwenye control number.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ikoje? Kuna wakati kijana amekusanya milioni tano anakwenda na milioni tano mkononi, anapewa control number yenye thamani ya milioni moja. Tukiwauliza watu wa ICT wanakwambia mfumo upo down hauwezi ku-take up taarifa zote. Hili ni tatizo kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna baadhi ya Waheshimiwa Wabunge hapa wamechangia kwamba mwezi mzima mfumo uko chini malipo mbalimbali hayafanyiki. Kwa kweli tunatambua umuhimu wa mfumo huu wa ukusanyaji wa mapato, lakini na mfumo ambao unatumika kwenye malipo. Hata hivyo, nimshauri Daktari, nadhani sasa anahitaji kuja na mkakati rasmi wa kuhakikisha kwamba tunawezaje kuboresha huu mfumo wetu kwenye malipo na kukusanya mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kuhusu huu mfumo wetu, mfumo huu ni mzuri sana, lakini nadhani kuna sehemu ambazo mess up. Inakuwaje wiki mbili mfumo uko down lakini hatuwezi kulipa? Kwa hiyo Mheshimiwa nimwombe Waziri akae na watu wake wa Wizara ya Fedha, watu wa IT kwa kushirikiana na BOT watuambie, tunawezaje kuufanya mfumo huu uwe user friendly na watu walipe kwa wakati?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa vijana wanapokusanya mapato hawatakiwi kukaa na fedha nyingi. Risk ikoje? Kijana amekusanya milioni tano anapokwenda kuomba control number aka–bank zile fedha anatolewa control number ya milioni moja, milioni nne anarudi nayo. What happened kwa Manyoni? Ilifika kipindi sisi tulikuwa na defaulters zaidi ya milioni 100 kwa mwaka. Watu ambao ukiwauliza hii hela mbona unadaiwa haamini kama anadaiwa. Kumbe kipindi kile alitolewa control number yenye value ya chini akajua labda hawa watu wamesahau ile milioni nne akaa nayo, muda ukaenda akaamua kuitumia. Hili ni tatizo kubwa. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Waziri, kwenye huu mfumo wa kukusanya mapato ambao wmeuanzisha sasa hivi wa TAUSI namshauri waende wakafanye maboresho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze TAMISEMI na Waziri wa Fedha, wameboresha huu mfumo wa zamani wa kukusanya mapato wamekuja na huu mfumo mpya ambao unaitwa TAUSI ambao halmashauri nyingi zimeanza kuutumia, lakini bado kuna changamoto moja. Mfumo huu unahitaji elimu itolewe kwa wananchi. Kwa mfano sasa hivi, business license zote zinatolewa kwenye mfimp wa TAUSI kila kitu, mfanyabiashara, fundi anatakiwa ajisajili kwenye mfumo wa TAUSI, ni wangapi wanaujua huu mfumo? Tunahitaji kutoa elimu kwa wananchi ili waujue huu mfumo na iwe rahisi ku–take off tunapoanza ile Julai kwa zile halmashauri ambazo bado hazijaanza kuzitumia ili ziweze kuutumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwenye huu mfumo wa kutoa control number, kama kijana anaweza akakusanya milioni tano anapokwenda anakuta system iko down au inatoa bili ambayo iko chini, ningeshauri watengeneze back up system kuliko hawa vijana kukaa na hela muda mrefu, inakuwa ni very risk kwao. Matokeo yake tunawaingiza kwenye risk ya kudaiwa na tunakuwa na defaulters wengi. Kwa hiyo nashauri waandae back up system ambapo kama mfumo uko down hawa vijana wasikae na fedha nyingi nyumbani tuwe na mfumo ambao tunaweza kwenda ku–bank, then wakafanya reconciliation. Lengo ni kuhakikisha kwamba tunapunguza misuse za fedha, lakini pia tunapunguza upotevu wa hizi fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo nataka kuchangia ni kuhusu miradi mikubwa ya maendeleo. Niishukuru sana Serikali, kwa Manyoni tumepata fedha nyingi sana. Tumepewa bilioni nne za Ujenzi wa Shule ya Wasichana ya Mkoa. Vile vile, tumepewa zaidi ya bilioni moja kwa ajili ya Ujenzi wa Chuo cha VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu anatambua Daraja la Sanza. Kwenye kila Ilani ya Uchaguzi huwa Daraja la Sanza linawekwa. Nafahamu sasa hivi lipo kwenye mchakato wa manunuzi. Nimwombe Waziri mwaka unapoanza sasa, huyo mkandarasi akapatikane na ujenzi wa daraja la Sanza uweze kuanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili na Mheshimiwa Waziri anatambua kuna Mradi pale Mwahalala, Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi wa Magari. Ule Mradi wa zaidi ya bilioni 30 ulisimama tangu mwaka 2016. Pale kuna majengo yanaendelea kuoza. Sasa ningeshauri kwenye bajeti hii ingawa sijaona anapoelezea, naomba Waziri anapokuja ku–wind up atuambie, nini mpango wa Serikali kuuendeleza ule mradi ambao umesimama tangu mwaka 2016.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale kuna nyumba, tunashauri kama Serikali imeacha huu mradi waturuhusu zile nyumba zitumiwe na watumishi. Tuna Shule za Sekondari, Shule za Msingi, zahanati, nyumba zile zinaweza zikatumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, kuna huu Mradi wa Mji wa bilioni 12 wa Kintinku-Lusilile. Kwanza, namshukuru sana Waziri wa Fedha, kwa kweli kwenye huu mradi ametusaidia sana na sasa hivi mkandarasi yuko site ameanza kazi. Hata hivyo, bado mkandarasi anadai zaidi ya bilioni tano ili aweze kukamilisha huu Mradi. Kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Waziri, kwenye huu mradi ambao unakwenda kwenye vijiji 11 ambao una zaidi ya miaka 15 haujakamilika, atusaidie ili uweze kukamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, niendelee kumpongeze sana Mheshimiwa Rais, lakini nimpongeze Mheshimiwa Mwigulu na timu yake na naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)