Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya wananchi wa Serengeti naomba nichukue nafasi hii kuchangia Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti naomba nianze na Mawasiliano. Katika Wilaya ya Serengeti tuna maeneo mengi sana ambayo mitandao ya simu hakuna na tunavyoongelea Serengeti, ndiko kwenye mbuga ambayo inaingiza fedha nyingi katika nchi hii, yaani ndiyo mbuga ambayo inasaidia ku-finance watumishi wa TANAPA kwenye mbuga nyingine kama Mikumi na maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mbuga hii kuna maeneo mengi ambayo hayana mawasiliano. Kwa mfano Robo ambako kuna Hoteli ya Robo hakuna mawasiliano kabisa, Bilila iko shida. Mheshimiwa Waziri nikuombe wakati wa ku-wind up hebu njoo na jibu la kueleweka kwamba sasa hoteli ambazo ziko ndani ya hifadhi watapata minara kwa ajili ya mawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni barabara. Sasa naomba niseme kuhusu barabara ya Makutano – Nata – Mugumu – Loliondo – Mto wa Mbu. Aliyeanza kuwa na maono ya kujenga barabara hii ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, wakati huo ikiitwa Makutano – Nata – Ikoma Gate.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baadaye alipokuja Mheshimiwa Benjamin William Mkapa ndipo wakaanza kuiweka kwenye Ilani ya CCM. Mkapa akaondoka, katika miaka yake kumi hakujenga barabara hii. Akaja Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, ikawekwa kwenye Ilani ya CCM, wakati huo Mheshimiwa John Pombe Magufuli akiwa ndiye Waziri wa Wizara ya Ujenzi. Ikapita miaka kumi wala hakuna chochote kilichofanyika. Sasa amekuja ambaye alikuwa Waziri wa wizara hiyo, Mheshimiwa John Pombe Magufuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni barabara pekee inayounganisha Mkoa wa Mara na Mkoa wa Arusha. Wakati mwingine watu wa Mkoa wa Mara wanalalamika hawanufaiki na utalii, hawanufaiki na fursa zilizopo za utali, ni kwa sababu barabara hii haijafunguka kuunganisha mkoa wa Mara na mkoa wa Arusha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni aibu sana, barabara hii mwaka 2013 ilitengewa fedha kwenye bajeti ili ianze kujengwa na mwezi wa tatu mwaka 2013 ujenzi wa barabara ukaanza, ambapo wakandarasi wa ndani ndio waliokuwa awarded tender ya kujenga barabara hii. Na bahati nzuri mmoja wa wakandarasi anaitwa Steven Makigo, rafiki yake sana Magufuli, akapewa kazi ya kujenga barabara hii. Yeye na wenzake contractors kumi, tangu mwaka 2013 mwezi wa tatu mpaka leo ninavyoongea wamepewa shilingi bilioni 14 hawajajenga hata mita moja ya lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia; waliopewa kujenga barabara hii ya lami, Makutano – Nata – Mto wa Mbu ni contractors wa ndani wakiongozwa na Kampuni ya Mayanga ambayo Mkurugenzi wake ni huyu Steven Makigo, wako contractors kumi. Wakaisajili kwa jina moja wanasema Mbutu Bridge Contractors; ni wa kwetu ni wazawa. Tangu 2013 wamepewa shilingi bilioni 14 hata mita moja ya lami hakuna halafu mnasema hapa kazi tu, hapa kazi kwa issue gani? Kama mmewapa bilioni 14 wameshindwa wanyang‟anyeni, watumbueni majipu wale, anzeni na huyu mkandarasi, yaani hakuna chochote anachofanya lakini munampa mahela tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siku moja nimeuliza swali hapa Mheshimiwa Waziri hakulijibu na hiyo wamepewa kujenga 50 kilometers kuanzia Makutano mpaka Sanzate. Sasa hivi ninavyoongea mkataba wa kujenga barabara ile uliisha mwaka 2015 mwezi wa tano, baadaye wakaomba extension wakaongezewa mpaka Machi 2016, hivi huu ni mwezi gani? Mpaka leo bado hawajajenga hata mita moja, bado tunaendelea ku-entertain watu wa namna hii, si afadhali mtuwekee pale Mchina ajenge ile barabara ikamilike haraka.
KUHUSU UTARATIBU...
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee, kwa kanuni aliyoisoma; inasema hatatumia jina la Rais kwa dhihaka katika mjadala au kwa maudhui ya kutaka kulishawishi Bunge kuamua jambo lolote kwa namna fulani kwani mimi nimewashawishi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naombo niendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi simuongelei Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, namuongelea yule aliyekuwa Waziri wa Ujenzi wakati huo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni aibu, kama watu wamepewa shilingi bilioni 14 hata mita moja ya lami hawajajenga halafu unaniambia nisiongee, I have to talk. Nimeletwa hapa kama Mbunge wa Jimbo la Serengeti niongee kwa niaba ya wananchi wa Serengeti. Tunachokiongea hapa si mambo ya chama, hata kama ingelikuwa kwako wewe wametumia shilingi bilioni 14 hawajajenga kilometa moja ya lami utasikia vizuri, au huyo malaika akiguswa mnasikiaje? Tulia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni yenyewe sasa hivi wanajenga daraja la Mto Kiarano, hata structural engineer hawana, material engineer hayupo! Hivi hii Wizara ikoje hii?
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, haina watu wa kwenda kukagua pale waone kwamba kuna structural engineer, material engineer? wataalamu wa namna hii hawapo? Sasa unajenga barabara ya kuunganisha mkoa na mkoa key personnel are not there, ninyi vipi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi nataka Waziri anapokuja atuambie hii barabara itakamilika lini? Kwa mwendo huu ndiyo mtatuambia hapa kazi tu, hakuna cha kazi hapa tunadanganyana. Na kama kweli Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli anaipenda nchi hii, anawapenda wananchi wa Mkoa wa Mara, anawapenda wananchi wa Serengeti, aanze ku-deal na huyu mkandarasi. Kama mtu anaweza kutumia shilingi bilioni 14 halafu hakuna chochote alichofanya halafu watu wanaona sawa tu eti usimguse nitakugusa tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Mara tumesema ni mkoa ambao ni very potential, una mbuga ya wanyama, una migodi ya Nyamongo, tuna watalii na watalii wengi kama mnavyojua wanatokea uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta – Nairobi, wanapita Sirali, Tarime wanakuja Serengeti. Ninavyoongea kwa sasa barabara zote Serengeti zimekatika na tunaelekea kwenye high season, sijui hata hayo mapato tunayoyategemea kutokana na utalii tutayapata wapi kama barabara zimekatika inakuwa ni chaos kwa watalii?
Mheshimiwa Maghembe uko hapo unafahamu, watalii wengi wanatokea Nairobi, sasa kama hatutaki kujenga hata barabara ya Tarime - Mugumu watalii watakata tamaa. Kuna Barabara ya Musoma – Sirori Simba, Magange Ring‟wani ya kuingia Mugumu, barabara zote hizo hazina hata lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Serengeti ndiyo wilaya pekee ambayo mtoto anaweza akazaliwa akasoma Shule ya Msingi Ring‟wani akaenda sekondari ya Ring‟wani akamaliza akaenda form six pale Nata sekondari, akasoma Chuo cha Kisare hajawahi kuona hata lami. Ni Wilaya pekee ya kitalii ambayo haina hata mita moja ya lami…
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi namuomba Mheshimiwa Waziri…
MWENYEKITI: Muda wako umemalizika Mheshimiwa Marwa!