Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi ya kuchangia.

Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu mwenye enzi na utukufu kwa kuniwezesha kusimama mahali hapa muda na wakati kama huu. Nichukue fursa hii pia kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuboresha hali ya maisha ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika kazi kubwa amefanya katika Wizara mbalimbali, katika Wizara hii ya leo mahsusi kabisa hakika Mama amefanya mengi ambayo tunapaswa kuyasemea vizuri bila woga kabisa. Mama amefanya ubunifu katika suala zima la kumalizia mradi mkubwa huu wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pia ameongeza ubunifu mkubwa katika usambazaji, usafirishaji wa umeme nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika nimeisikiliza vizuri hotuba ya Mheshimiwa Waziri, hotuba hii imesheheni mikakati mizuri na mikubwa ambayo Serikali wameipanga kuhakikisha kwamba tunakwenda kupata umeme wa uhakika. Niwaombe ndugu zangu Wabunge mapungufu madogo madogo yaliyokuwepo kwa mikakati hii iliyotajwa leo, ninahakika inakwenda kuisha kabla ya kufika 2025. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasema hivi kwa sababu gani? Sasa hivi shirika la umeme nchini linauwezo wa kufua megawatt 1822 mpaka kufikia Mei, 2023 mahitaji halisi ni 1431. Maana yake TANESCO kwa uboreshaji wa mitambo iliyokuwa chakavu sasa inakwenda kuzidi kiwango kinachotarajiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, nimepita kwenye banda pale nimeona kwenye real time display majira ya saa nane mchana, umeme ulikuwa unazalishwa megawatt 1,426 na vituo vyote kuanzia Mtera, Pangani, Kihansi, Hale mitambo yote ilikuwa on time inafanya kazi zake sawa sawa. Vilevile, hata mashine sita za Songas zote zinafanya kazi vizuri sasa hivi. Ni mashine moja tu pale Songas ndiyo inafanyiwa matengenezo na pale kwetu Hale mashine moja tu ndiyo ambayo ilikuwa haifanyi kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niiombe Serikali ifanye hima na kumalizia matengenezo katika kituo cha Hale, vilevile na ile mashine moja ya pale Songas iweze kuzalisha umeme ipasavyo. Naiona dhamira kubwa na njema ya Serikali yetu kuhakikisha tunapata umeme wa uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nisemee kidogo mradi unaoendelea wa Bwawa la Mwalimu Nyerere. Hakika juzi nimepita kwenye Boots zile za nishati na nimeweza kushuhudia mradi ule kupitia Visual video ya mradi ule mzima. Hakika binfasi nime–fall in love with that project. Hakika natamani nipate kama siku tatu au nne niende nikatembelee mradi ule. Ni mradi mtamu sana kwa mafundisho makubwa ya Taifa letu na ni mradi wa kihistoria kabisa. Ninaiomba sana Serikali na hii naamini ni shemu ya contract administration, tuhakikishe kwamba material yote yaliyotumika katika mradi ule yanahifadhiwa mahali maalum, iwe kama ni museum ya mradi ule kwa ajili ya vizazi vijavyo kuendelea kujifunza kwenye bwawa lile, nina hakika hata kwa ajili ya future maintenance program, material zile zilizotumika sasa zikihifadhiwa vizuri itajulikana kwa urahisi zaidi kwa ajili ya matengenezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona wenzetu wa hitches on bridge wameweza kufanya museum ambayo kila anayekwenda anaona material yote ya mradi ule ulivyotengenezwa lakini kama ninyi ambavyo mmeonesha ubunifu wa cameras zile ambazo tumefanya visual observation ya mradi ule vilevile, na wao wameweka darubini ambayo mtu anaweza akaingiza hela pale na akawa anaona hitches on bridge jinsi ambavyo ina-operate. Kwa hiyo, kwa namna hiyo tunaweza tukapata hela ndogo ndogo kwa ajili ya kufanya utalii wa ndani kupitia mradi ule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumeona Aswan Dam ya Egypty, tumeona Akasombo Dam ya Ghana, wenzetu wanatumia Dam zile kiutalii pia. Niombe sana Kaka yangu naamini ubunifu wako, umeonesha makubwa ndani ya kipindi chako na hili mkashirikiane na Wizara ya Maliasili na Utalii tuweze kupata utalii wa ndani kwa maana ya kupata boat tuweze ku–sell around the dam na tuweze ku–enjoy neema kubwa ambayo Mwenyezi Mungu ametupatia katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, inapendeza zaidi kwa sababu tayari kuna mbuga ya Mwalimu Nyerere katika eneo lile, ni nafasi nzuri kabisa ya kutengeneza kind of resorts ndani ya maeneo yale ili kuweza kuvutia zaidi watalii na liingizwe bwawa lile katika utalii wa Afrika. Kwa sababu ni bwawa ambalo naamini kwa ukubwa litakuwa ndilo la pili ukitoa la Ethiopia. Wenzetu wa Egypt ambao wanatujengea nao tumekwishawapiga chini, wapo na 2110 sisi tuna 2115. Kwa hiyo, ni mradi wa heshima ni mradi wa kihistoria kwa Taifa leu. Ninawapongeza sana Serikali kwa juhudi kubwa mnazozifanya kuhakikisha mradi huu unakamilika vizuri na hakuna longo longo pigeni kazi, msiogope maneno ya wanaosema, kazi yenu inaonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kaka yangu January nikutie nguvu na nikutie moyo kwamba katika Quran sura ya 41 katika ayatul hashir inasema hivi “Tahsabuhum Jami’an wa qulubuhum Syattaa” utawaona watu wameunganisha nguvu kama vile ni wamoja lakini nyoyo zao zina uadui. Wanaunganisha tu nguvu ili wa defeat the strong, you know you can’t strengthen the weak by weakening the strong. Kwa hiyo, Kaka yangu nikwambie piga kazi, kazi yako ni kubwa na mimi nimeielewa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii pia kuipongeza Serikali kwa kutuletea transformer ya megawatt 55 pale katika kituo cha Majani mapana. Kazi hii tunaishukuru sana Serikali kwa sababu wale wawekezaji na wenye viwanda waliokuwa wakilalamika kwa sababu ya low voltage tatizo hilo Tanga linakwenda kuisha kabisa. Naomba kutumia fursa hii kuwambia wawekezaji popote walipo karibuni Tanga, tuna uwezo mkubwa wa umeme wa kuhudumia viwanda vyote vya Tanga vilivyopo sasa hivi na hata viwanda vingine vijavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashukuru sana kwa transformer ile ambayo sasa hivi imekwishafika site na inafungwa bado tu Commissioning. Tunashukuru sana Serikali, Watendaji wa TANESCO, Ndugu yangu Maharage kazi yako ni njema, mmejipanga vizuri na sisi tunaona. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika nakumbuka kuunganishiwa umeme ilikuwa inachukua mpaka miezi mitatu, chini ya uongozi wa Maharage sasa hivi baada ya kulipia umeme unakufikia nyumbani ndani ya siku nne. Ni mapinduzi makubwa ambayo Watanzania tunapaswa kuwapa nguvu na moyo ndugu zetu hawa ambao wana nia njema ya kuliendeleza Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niwapongeze Serikali nimeona mmetenga fedha kwa ajili ya gridi imara, ni jambo kubwa ambalo litaimarisha umeme wa maeneo yetu. Kule Simiyu, Ruvuma, Kilindi kote tunakwenda kunufaika na mradi huu wa gridi imara. Hakika ninayaona mapinduzi makubwa katika sekta hii ya nishati kwa uboreshaji huu wa gridi imara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, ahsante sana. (Makofi)