Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. PETER A. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naitwa Peter Lijualikali, siyo Juakali. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kutimiza jukumu langu la Kikatiba kuwepo mahali hapa na nitaanza na TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mpango wa kuisaidia miji ili iweze kuendelea nimeona hapa kuna miji 18 ambayo Mheshimiwa George Simbachawene ameiweka kwenye hotuba yake, kwenye hii miji siuoni Mji wa Ifakara, ni mji mpya ambao ninadhani kwa changamoto ambazo mji huu unao kama za barabara na juzi tulikuwa na mafuriko makubwa sana ambapo Mto Rumemo umekuwa na kawaida ya kumwaga maji kuja Mjini Ifakara, sasa nimeshangaa tangu bajeti ya 2016 miji ni ile ile 18, kuna miji mipya mwaka jana imetangazwa na Ifakara ikiwemo, lakini mji wangu wa Ifakara hauonekani kwenye huu mpango.
Sasa nichukue wakati huu kumuomba Mheshimiwa Waziri Simbachawene aweze kukumbuka Mji wa Ifakara kwa maana ni mji mpya, mji ambao una changamoto, ningependa kuona unaingia kwenye huu mpango ili mji uweze kwenda vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite kwenye suala lingine la utawala bora na hapa nitasema kidogo. Mwaka jana wakati tunakwenda kwenye Uchaguzi Mkuu, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na mara zote tumekuwa tukisema Tume hii siyo huru na mfano hapa upo; kwamba Tume ya Uchaguzi ilikuja Ifakara, Kilombero ilikuja kuhakiki majimbo mapya na huu ni mpango wa kila baada ya miaka mitano. Mwenyekiti wa Tume hii akasema Ifakara kwa kuwa ni Halmashauri ya Mji ina-qualify automatic kuwa Jimbo la Uchaguzi, sehemu ikishakuwa Halmasahauri maana yake ina-qualify kuwa Jimbo automatic. Kile kigezo cha population hapa hakipo tena kwa sababu hii ni mamlaka inayojitegemea. Kunakuwa na Baraza la Madiwani, Halmashauri, Mkurugenzi na Idara kamili which means ina-qualify kuwa na Mbunge hapa sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Jaji Lubuva kukiri kwamba Ifakara ina-qualify kuwa jimbo nikashangaa anakuja kutangaza majimbo mapya Ifakara haipo. Nikashangaa sana na nikasema kama Serikali ya CCM inaongoza mambo yake kisheria na kwa miongozo ya Katiba ni kwa nini Ifakara iachwe, wakati sheria na vigezo vya Ifakara kuwa Jimbo vilikuwa vinaipa Ifakara kuwa jimbo. Na nikasema kama Tume ya Uchaguzi inao wataalam, ina wanasheria na wanajua fika kwamba Ifakara ina-qualify kuwa jimbo lakini kwa makusudi wakanyima Ifakara kuwa jimbo tafsiri yake ni nini? Tafsiri yake ni kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi siyo huru, haifanyi kazi zake kisheria ni uhuni unaofanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho tumekuwa tukisema upinzani kwamba hii Tume hii irekebishwe nafikiri kuna haja ya hii kitu kufanyiwa kazi na katika mazingira kama haya kama Tume inakubali kabisa kwamba Ifakara inapaswa kuwa jimbo halafu wanashindwa kulifanya jimbo kwa nini tusikubali kwamba pia Lowassa mlimwibia? (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kitu kipo wazi, yaani kitu kipo wazi tu kisheria kwamba hii sehemu inafaa kuwa jimbo Mwenyekiti wa Tume anakubali kwamba hii sehemu inafaa kuwa jimbo lakini anafanya lisiwe jimbo kihuni tu, kwa nini tusikubali kwamba Tume hii CCM mmekuwa mkiitumia kihuni ili mfanikiwe ninyi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana kwenye hii hii utawala bora yametokea mpaka mimi nakuja kukamatwa na polisi wananikwida kwa sababu ya huu uhuni leo eti polisi mwenye ā€žVā€Ÿ koplo anakuja kumkamata Mbunge kihuni kabisa. Leo hii kila mtu anasema Lijualikali ulionewa unastahili kwenda Kilombero na bahati yangu kwenda Kilombero nazuiwa na polisi na nina kesi mahakamani kwa sababu hiyo, halafu mnasema eti hapa kuna utawala bora!Huo utawala bora uko wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo ambayo nadhani Taifa hatupaswi kuyaendeleza. Ninadhani tuna kila sababu ya kurekebisha siasa zetu. Kama sehemu inastahili haki zake sehemu inastahili na haya unakuta hata katika Mkoa wa Dar es Salaam, Madiwani wengi ni wa UKAWA, lakini Serikali ya CCM mmetafuta namna zozote mnazoziweza ili mshinde Jiji. Mmefanya kila namna mnahangaika, mnajua kabisa hamna haki hiyo, lakini mnahangaika mnavyoweza ili muweze tu kushinda.
TAARIFA....
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli unabaki pale pale kwamba tumetumia miezi mitano, tumefanya vurugu, mpaka zimekuwa forged hati za mahakama ambazo mahakama imekataa. Nabaki kwenye msingi ule ule kwa nini mpaka mahakama isingiziwe? Kwa nini mpaka tufike huko?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nimekosea kusema Rais, na Rais anisemehe sana na ninyi mnisamehe lakini nina hoja ya msingi hapa, hii hoja hatuwezi kuidharau, kwa nini mpaka tufikie huku? labda nimesema hivi kwa sababu nimekwazwa moyoni, nimeumia moyoni yaani ni kwa nini nifanyiwe hivi, Rais yupo, Waziri Mkuu yupo, mpo wote kwa nini vitokee hivi? Kwa hiyo, ni kweli naomba mnisamehe, najua mnajua kwamba mlikosea na Mungu awasamehe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye hoja nyingine, kuna kitu...
MWENYEKITI: Mheshimiwa muda umeisha jamani.
MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo ndiyo nimeyasema sasa hivi hapa, this is not fair, haya nimeyasema sasa hivi tu, ameongea mbele yangu muda amechukua hapa na umeona kabisa, ndiyo nimesema sasa hivi mambo haya, hamsikii tunasema hapa ndani lakini hamsikii, hatuwezi kwenda hivi kama Taifa!