Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumshukuru Mungu kwa kunipa pumzi ya uhai, pia nachukua nafasi hii kumpongeza Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi zake anazozifanya kwa kasi Sana kwa kipindi kifupi, aidha nikupongeze wewe kwa kuendesha Bunge letu kwa weledi mkubwa pasipo kupindapinda.

Mheshimiwa Spika, naomba kupongeza pia juhudi za Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa pamoja na Jenerali Jacob John Mkunda, pia nampongeza Luteni Jenerali Salum Haji Othman kwa kupandishwa cheo na kuteuliwa kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi letu.

Mheshimiwa Spika, nina ombi kwa Serikali yetu Sikivu, kuna maeneo katika Wilaya ya Nachingwea ambayo baada ya ku- review mipaka ya Kikosi cha Jeshi Majimaji yalichukua maeneo ambayo yalikuwa yanamilikiwa na wananchi wa Nampemba kwa miaka yote tangu enzi za mababu na mababu.

Mheshimiwa Spika, maeneo yale wazee wetu wengi wameweka mashamba ya mikorosho ambayo yanawapatia riziki kwa miaka yote. Ombi langu kwa Serikali kwa kuwa wameyachukua yale maeneo na watu wameyahudumia na kuwa tegemeo la maisha yao, naomba sana wale watu wafikiriwe wapewe hata kifuta jasho kwa kuwa maeneo hayo yalikuwa ni tegemeo kwa maisha yao.

Mheshimiwa Spika, ombi lingine ni kwa wananchi wanaozunguka maeneo ya JKT Nachingwea; maeneo kama ya Mapochelo, Mkukwe na mengineyo nao pia wameathirika sana baada ya kupanua na ku-review maeneo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Nachingwea niombe sana Serikali yetu ijitahidi kuwapa kifuta jasho wananchi wale.

Mheshimiwa Spika, wananchi wale yale maeneo yalikuwa ni tegemeo lao katika kuendesha maisha yao, niombe sana wananchi hawa wa maeneo haya ambayo nimeyataja wapewe kifuta jasho ili waweze kwenda kutafuta maeneo mengine ya mashamba kwa ajili ya kuendeleza maisha yao.

Mheshimiwa Spika, najua Serikali yetu ni sikivu ijitahidi kuwasaidia wananchi wale wako kwenye hali mbaya sana.

Mheshimiwa Spika, ombi langu lingine ninaomba Kikosi cha Jeshi Farm Seventeen kilitunza viongozi wengi sana waliokuwa wanapigania uhuru nchi za Kusini mwa Bara la Afrika, niombe Serikali yetu ikumbuke maeneo yale kufanya matengenezo na marekebisho kwa kuwa yamekuwa machakavu sana.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.