Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika hoja iliyo mbele ya Bunge lako Tukufu. Nitumie nafasi hii kuwashukuru wananchi wa Buchosa, kwa kunirudisha tena katika chombo hiki cha uwakilishi hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niipongeze na kuishukuru Serikali kwa kazi nzuri wanayoifanya. Binadamu sifa yake kubwa ya kwanza ni kushukuru kwa jambo linalofanyika vizuri; lakini itakuwa ni udhaifu mkubwa sana pale ambako jambo unaliona linafanyika vizuri unajitoa fahamu, unapewa dakika 10 za kuchangia hapa ndani, wewe unaanza kurusha maneno mabaya tu, like waliokutoa huko kukuleta hapa; moja ya ajenda ilikuwa ni kukutuma uje kutukana.
Waheshimiwa Wabunge, hebu tutimize wajibu wetu juzi Attorney General hapa akizungumzia habari hii ya live coverage ya Bunge na kadhalika; alisema hebu kwanza tujiongoze na wajibu wetu tu wa Kibunge wa kawaida and then haya mambo mengine yata-follow in place. Ndugu zangu Mabunge yaliyopita wengi walizungumza sana humu wakahutubia Taifa sana. Halafu leo hawamo wote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ningeomba sana tushiriki mijadala hii pale kwenye kuwezekana kukosoa, tukosoane ni kweli; lakini tusiendeleze drama zile za kutafuta umaarufu kupitia runinga na mambo ya namna hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yako makelele haya ya television na kadhalika, Mheshimiwa Nape amejitahidi sana kulielezea hili jambo. Nataka niwape hadithi tu ndogo siku tunatambulishwa, niko katika Kamati ya Huduma za Jamii, siku tunatambulishwa, Kamati hii na Wizara msemaji mmoja wa upande huo huko, akasema yeye hakumbuki mara ya mwisho yeye na familia yake wame-tune TBC lini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nikamtazama yule bwana nikamuuliza hivi wewe utaratibu huu unadhani ni sifa? Nashangaa juzi kabadilisha, baniani mbaya… Samahani bwana baniani uliyemo humu; kabadilisha utaratibu, baniani mbaya huyo TBC sasa amekuwa dawa. Anamtaka humu ndani kwa udi na uvumba. Guys! mnaweza mkafanya unafiki, lakini huu unapitiliza.
falsafa ya Wachina kwamba ukiona Wapinzani umefanya jambo wanapiga yowe kanyagia hapo hapo. Ukiona unafanya jambo wanakupongeza kwa kweli hilo achana nalo haraka sana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri Mkuu, haya mnayoyafanya kanyagieni hapo hapo. Ukiona wana shift position hawa ujue mambo yamewakaa vibaya. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu mwingine utakuwa katika maeneo mawili yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, ni katika Sheria ya Mfuko wa Barabara. Sheria hii sasa ina miaka kama 17 hivi tangu ianze kutumika, lakini kuna mambo mengi yamebadilika hapa tangu sheria hii ianze kutumika na kwa kweli dhana iliyokuwa wakati ule kwamba Serikali za Mitaa hazikuwa na uwezo mzuri wa kusimamia hizo fedha, haiku valid tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia Mheshimiwa Shabiby asubuhi, wakati akichangia akipendekeza utazamwe upya mgawanyo wa hizo fedha, asilimia 30 kwa 70; kama ilivyo sasa inazisababisha halmashauri na hasa sisi Wabunge wengi kuomba barabara zilizo chini ya halmashauri zipandishwe hadhi kuwa barabara za mikoa. Sasa hili tunaweza kuepukana nalo, kwa sababu hatuwezi kuendelea hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, naomba tulitazame hili jambo, tukiendelea hivi eventualy barabara zote zitakuwa za mikoa siyo? Kwa sababu kila mwaka tunaendelea ku-upgrade. Kwa hiyo, nadhani kwamba tufike mahali sasa tukubaliane, ile percentage inavyogawanywa, ibadilishwe ili kuzifanya Halmashauri na zenyewe ziwe na fedha za kutosha kufanya matengenezo yanayokidhi; huko huko katika Halmashauri bila kung‟ang‟ana kuzipandisha hadhi kuzifanya barabara za Mkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninalo andiko ambalo nitamkabidhi Waziri wa Ujenzi, ili aweze kuona ni kwa namna gani tunaweza kuhama kutoka kule bila kuathiri kiwango cha ubora wa matengenezo ya barabara za mikoa na barabara kuu. Tukilifanya hili tutakuwa tumefanya service kwa pande zote mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki niamini kwamba wako wahandisi wabaya katika Halmashauri zetu na wako Wahandisi wazuri katika Wakala wa Barabara wa Taifa. Wote hao wanasoma vyuo hivyo hivyo; tunachokiona tu hapa ni uwajibikaji na kiasi cha pesa ambazo mtu anakuwanacho katika ku-effect hizi kazi. Kwa hiyo, tuki-address haya mambo mawili nadhani tutaliondoa hili wingu na wimbi la kuomba barabara hizi kupandishwa hadhi kutoka barabara za Wilaya kwenda kuwa barabara za Mkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ambalo nataka kuchangia ni miradi ya maendeleo inayoanzishwa katika Halmashauri zetu. Ukitazama na Waheshimiwa Wabunge, watakuwa mashahidi; miradi mingi miaka mitatu, miwili iliyopita ilianzishwa kule, lakini katika bajeti zinazofuata miradi hii haipati tena pesa. Kwa hiyo, imebaki tu katikati na mfano mmoja wa haraka kabisa ni hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii Hospitali imeanza kujengwa mwaka juzi ilipata bajeti katika Serikali, mwaka jana haikupata pesa, mwaka huu wa fedha unaomalizika haikupata pesa.Lakini sasa Mheshimiwa Waziri mmeanzisha miradi mingine ya aina hiyo hiyo wakati hii iliyotangulia haijakamilika. Niombe sana hebu tu take stock kwanza ya miradi ambayo imekwishaanza ya aina inayofanana. Tuweke utaratibu wa kuikamilisha hiyo kabla hatujaingia kwenye kuanzisha miradi mingine mipya ya aina hiyo hiyo baada ya kukamilisha iliyokuwa imetangulia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine lililogusiwa pia asubuhi; kilimo, sasa sina hakika kama ni uvivu wa watendaji wetu katika TAMISEMI kule, lakini utaona mgawanyo wa fedha ambao umewekwa katika Wilaya mbalimbali inashangaza kidogo. Ameusema vizuri sana Mheshimiwa Shabiby; Dar es Salaam wilaya tatu zina milioni 360 hivi, mkoa mkubwa kwa kilimo kama Geita una milioni 143; hii si sahihi. Nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, hatujafika mwisho wa mchakato huu wa kuunda bajeti; hebu warekebishe hili jambo ili mipango hii i-reflect ukweli ulioko huko site. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu, vinginevyo tunakuwa sasa tunatanguliza toroli mbele ya punda halafu ni jambo ambalo si zuri sana. Wakati sisi humu tunaweza kuona na kufanyia marekebisho haya mambo. Niombe tu kwamba kwenye eneo hilo la kilimo litazameni sana fedha zilivyogawanywa na kama inawezekana mfanye mabadiliko haraka kabla hatujasonga mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo la mwisho; ni elimu. Elimu…
MHE. DKT. CHARLES J. TIZABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.