Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nataka nianze na utawala bora na habari zilizonifikia hivi punde ni kwamba Juliet Kairuki alikuwa Mkurugenzi wa TIC amefukuzwa kazi kwa sababu ya kutokupokea mshahara. Sasa ile bahasha aliyokuwa anasema msitulipe posho tunaweza tukapita kwenye wimbi hilo la kuvuliwa Ubunge kwa sababu ya kutokupokea posho. Naomba mliangalie vizuri kwa sababu utumbuaji wa majipu umeanza hata kama hupokei hela, this is very serious.
Mheshimiwa Naibu Spika, Rais aliyeko madarakani siyo kwamba kila anachokifanya hatukikubali, tunaiamini nia yake ya ku-restore glory ya nchi hii hasa baada ya sisi ndani ya Bunge hili kupiga kelele sana dhidi ya ufisadi katika Taifa hili. Anachokifanya Rais, siyo vitu vyote ni vibaya kwamba courage yake ya ku-restore glory kwenye utumishi wa umma siyo mbaya lakini utukufu binafsi unapozidi sifa za Mungu, Rais anaweza akakosea.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Rais, Dkt. Magufuli, kuteuliwa na chama chake kuwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi kulisababisha public opinion ambayo ilikuwa created na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu alionekana ni kati ya Mawaziri waliokuwa wakifanya vizuri katika Wizara zake ndani ya Bunge hili. Leo mmekuja na mapendekezo ya kuondoa live broadcasting ndani ya Bunge hili, maana yake leo tunaongea hatusikiki nje.
Mheshimiwa Naibu Spika, unaposema ni gharama Wabunge na Bunge kuongea na wananchi wao hizo gharama mna-compare to what? Yaani unaposema ni gharama kulipia matangazo ya Bunge wananchi wasikie Wabunge wanachojadili compared to what, expensive is a relatives. Leo mmekuja na mapendekezo mengine ya Wakurugenzi wa Wizara watoke na mabasi Dar es Salaam, waje Dodoma kwenye vikao sensitive vya Bunge. Mnafikiri ni kubana matumizi, huwezi kubana matumizi kwa kuondoa class, hiyo ni poverty mentality. Nchi hii ina rasilimali za kutosha ifikie mahali muanze kufikiria Wabunge kuja hapa na helicopter siyo Wakurugenzi wa Wizara kuja hapa na mabasi. Haya mambo tulifanya wakati nchi inapata uhuru leo mnataka kuturudishia mnasema ni kubana matumizi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, huwezi kubana matumizi kwa ku-create poverty mentality kwenye mfumo, huwezi kubana matumizi kwa kumfanya tajiri aishi kama maskini. Rais anatoa kauli, anasema hawa wanaoishi kama malaika wataishi kama mashetani, this is bad na mnashindwa kumshauri kazi ya Rais ni kufanya mashetani kuokoka waishi kama malaika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, huwezi kuwa na wish ya kufanya watu wako kuwa na maisha mabaya lazima uwe na wish ya kufanya watu wako kuwa na maisha mazuri. Sasa kinachoendelea sasa mnafikiri mnakomoa opposition; mnachokifanya mnamtengenezea Rais spirit of dictatorship, mnamfanya Rais anakuwa ni one man show game. Kama Rais angekuwa na nia njema ya ufisadi, kazi nyingi tungemsaidia hapa Bungeni. Kama Rais angekuwa na nia ya kupigana angeacha Bunge liwe live.
Mheshimiwa Naibu Spika, Rais mwenyewe anajua umuhimu wa vyombo vya habari kila anakokwenda amesema mwenzangu hapa anabeba TBC hata kama ana kwenda kufumania bahati mbaya kazini; unashangaa hawa Azam na wenyewe wamejuaje leo Rais anakwenda BoT? Kumbe ni mipango. Kama mnajua umuhimu wa vyombo vya habari acheni Bunge liwe huru. Mnasema Rais wenu anawajibika vizuri cheni basi haya mambo yawe huru.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo mmetoa hela za Bunge hapa mnaita utawala bora, mmeenda kukabidhi kwa Rais, Spika hajui, Spika naye anasoma kwenye WhatsApp, Spika anaangalia mko Ikulu; yuko anaumwa anasoma kwenye WhatsApp, mnafanya maamuzi ya fedha za Bunge bila kushirikisha Kamishina wa Bunge, utawala bora uko wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukitaka tumsaidie Rais ku-restore glory katika Taifa hili, chombo cha kwanza cha kumsaidia ni Bunge kuwa democratic, hili Bunge halina uhuru. Mawaziri waoga leo hakuna innovation kwenye Ofisi za Mawaziri, hakuna innovation kwa Katibu wa Bunge, kila mtu anaogopa, sasa kama hivi usipopokea mshahara unatumbuliwa. Hawa watu kule kazini wako hivi, walikuwa wanafanya kazi bila instrument, walikuwa ni Mawaziri vivuli, hakuna watu wanaobuni, watu wako hivi wanaogopa, maamuzi hayafanyiki kwa sababu mmeshindwa kumshauri Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, utawala bora siyo huu mnaoufanya nyie. Nilishawaambia hapa tena narudia leo, lengo la opposition siyo kutawala nchi hii, lengo la opposition ni pamoja na kuona mnatutawala vizuri. Ingekuwa haya mambo mnayofanya yanaharibu chama chenu peke yenu lakini hayaharibu Taifa letu tungewaachia kwa sababu pengine maisha yenu hayatuhusu lakini mkiharibu, mnaharibu maisha ya watoto wetu ndiyo maana tunapiga kelele. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo nchi inaenda haijulikani, leo hakuna kiongozi wa Serikali anakwenda kazini asitegemee kufukuzwa kazi, leo anakwenda Makonda anamsoma mtu hadharani, unasema nifukuze kazi ama nisifukuze? We don‟t live like that man hatuwezi kuishi hivyo, wale wana wazazi, wana-family, wana ndugu, watu wote wanafanya makosa lakini hauwa-treat hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa na wewe umepeleka hela kule Ikulu sijui nani angekutumbua. Ukachukua hela bila hata kumuuliza bosi wako na wewe hapo siku hizi ndiyo unajifanya zaidi ya Spika, yaani wewe ni kila kitu, mnafika humu mnawaamulia Wabunge, magari ya Wabunge hakuna mnampa Mbunge milioni, eeh tabu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri Muhongo alikwenda bandarini, akamuuliza yule mama nani amekwambia ufungue lile bomba? Mama akasema nimeambiwa na Waziri. Mkamfukuza aliyeagizwa na bosi wake mnaacha aliyeagiza; mnawaonea watu, mnanyonga watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nirudi kwako kaka yangu Simbachawene, umeongea kwenye television kwamba kuanzia sasa Halmashauri ndiyo zitakusanya mapato, hamjajiandaa …
Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hamjajiandaa. Leo kwa kazi moja ya parking system Arusha Mjini utahitaji watu 220, utawalipa kima cha chini, Pay as You Earn, NSSF, Bima ya Afya, mfanyakazi mmoja aliyekuwa anakusanya parking kwa Sh.80,000 kupitia private sector leo wataigarimu Halmashauri Sh.400,000/=. Mnakwenda kuua Halmashauri kwa sababu ya disengagement ya private sector, angalieni hili suala kwa umakini sana kuhusu private sectors.
Mheshimiwa Naibu Spika, Zanzibar. Mmemaliza uchaguzi mmeshinda mmepiga kura wenyewe mmelinda kura, mlichoshinda Zanzibar mmeshinda tena hapa, kwa ushauri wa Nape, mkionesha Bunge wanaonekana sana hawa. Zanzibar kesi haijaisha, msifikiri mko salama, iangalieni Zanzibar vizuri, ukiona unapiga mnyonge anakaa kimya, Mandela alisema hatafuti kichochoro anatafuta njia ya kujitetea.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie, kuna Mheshimiwa Mbunge mmoja aliongea habari ya Arusha kwamba uchaguzi tumeshindwa, huyo haijui Arusha. Kwanza hatujui anakaa wapi, analala wapi, kama hawezi kuwa na tathmini ya watu ambao anaishi nao kila siku Tanga, Dodoma, Dar es Salaam hawezi kuwa na tathmini ya mkoa. Mwaka jana Wenyeviti sita wa CCM waliniunga mkono mwaka huu tumefanya uchaguzi, tumewanyang‟anya CCM mitaa minne imebaki miwili. Sasa yule dada anasema CCM Arusha inaendelea vizuri kwa kasi ya Magufuli. Ajue kwanza maisha yake na mumewe na wapi anaishi ni Tanga, Dar es Salaam, ni Mara ni Dodoma na anaishi na nani? Akishajua anaweza akajua tathmini ya Mkoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.