Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia hotuba hii ya TAMISEMI na Utawala Bora. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha mimi binafsi kuingia katika Bunge lako Tukufu, lakini katika namna ya kipekee kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Kilwa Kaskazini ambao wamenipa dhamana hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na miundombinu ya barabara. Jimbo langu kwa ujumla miundombinu ya barabara ni mibovu na kwa sasa barabara nyingi hazipitiki na hasa zile barabara kutoka Nangurukuru kwenda Liwale, haipitiki, ni mbaya. Sasa hivi kutoka Nangurukuru kupitia Njinjo kwenda Liwale, hakupitiki. Hivyo, inalazimika wananchi wanaotaka kwenda huko watembee au wapite katika umbali wa kilometa zaidi ya 400, wakati kutoka Nangurukuru kwenda Liwale ni umbali wa kilometa 230. Naishauri Serikali ione uwezekano wa kujenga barabara hii katika kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuna barabara kutoka Njia Nne kwenda Kipatimo, nayo sasa haipitiki, ni mbovu. Barabara hii inapitia katika Tarafa ya Miteja na Kipatimo. Pia naishauri Serikali ione uwezekano wa barabara hii kuijenga katika kiwango cha lami.
MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu lipo katika ukanda wa Pwani. Ukanda wa Pwani una matatizo makubwa ya maji, lakini tunayo fursa ya uwepo wa Mto Rufiji. Naishauri Serikali ione uwezekano wa kujenga mradi mkubwa wa maji katika Mto Rufiji utakaosaidia vijiji na rarafa zilizopo katika Wilaya Rufiji na Jimbo la Kilwa Kaskazini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye afya. Huduma za afya katika Jimbo langu bado zinalegalega; huduma zinazotolewa ni hafifu, hakuna dawa katika zahanati, hakuna wahudumu. Tuna zahanati kama sita ambazo zimemalizika kujengwa, lakini hazina dawa wala wahudumu, kama zahanati ya Mwengei, Luyumbu,Marendego, Kipindindi na Nambondo na Hongwe. Zahanati hizi zimemalizika kujengwa lakini mpaka sasa hivi hazijaanza kufanya kazi. Naiomba Serikali iangalie hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Jimbo langu kuna Hospitali moja tu, hospitali ya Mission. Hospitali hii haina x-ray na tayari wafadhili wa hospitali hii walitoa mashine ya kisasa ya x-ray, lakini kwa bahati mbaya kwa sababu ilichukua muda kupata jengo, ilipata hitilafu na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kusaidia kufanya ukarabati wa x-ray hii. Kwa bahati nzuri ilipofikia mwaka 2013 akatoa shilingi milioni 40 kufanya ukarabati wa x-ray hii. Mpaka sasa ninapozungumza x-ray hiyo haijakarabatiwa na pesa zile zipo. Naiomba Serikali ifuatilie ili basi wananchi wangu waweze kupata huduma ya x-ray.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu la Kilwa Kaskazini ni dampo la mifugo kutoka Mikoa ya wafugaji. Sasa hivi tuna tatizo kubwa la migogoro ya ardhi, lakini mapigano kati ya wakulima na wafugaji na ni kwa sababu tu wafugaji wote wanaotoka katika Mikoa ya wafugaji wanakuja katika Jimbo langu na kusambaza mifugo yao bila kufuata utaratibu wa matumizi bora ya ardhi.
Naiomba Serikali ihakikishe kwamba inaondoa mifugo yote ambayo ipo katika vijiji ambavyo havikupangwa kuwepo kwa mifugo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni elimu. Tunao mpango wa elimu bure. Huu mpango mpaka sasa naona bado ni kama unalegalega. Mimi binafsi nashauri mpango wa elimu bure uendane sambamba na kuangalia maslahi mapana ya walimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bure inazungumzia namna ya kumsaidia mwanafunzi, lakini bado haijamwagalia mwalimu. Napendekeza, mpango huu uendane sambamba na kuangalia uwezekano wa kutoa teaching allowance kwa walimu. Walimu wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu, ni vizuri sasa kuangalia maslahi yao. (Makofi)
Mheshimia Mwenyekiti, pia kuna majengo ya Shule na Ofisi za Serikali yanajengwa chini ya viwango. Majengo mengi yanayojengwa sasa, hayawezi kudumu hata kwa miaka kumi, hali ya kwamba majengo ya Serikali yanatakiwa ya kudumu kwa miaka 50 na kuendelea. Serikali iangalie uwezekano wa kusimamia ili majengo yanayojengwa sasa yawe ya kudumu kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la uhakiki wa Watumishi. Suala hili katika eneo langu limezua adha na kuna shida! Tayari Serikali ilifanya zoezi hili kwa mara ya kwanza, lakini sasa inaonekana ni lazima warudie tena kufanya tena kwa mara nyingine. Sasa inawagharimu wafanyakazi. Kwa mfano, wananchi wanaotoka Kijiji cha Nandete kwenda Kilwa Masoko ni ziaidi ya kilometa 140. Mtumishi huyu tayari alishakwenda kwa zoezi hilo kwa mara ya kwanza, lakini analazimika tena aende kwa mara ya pili. Hii inawasumbua sana watumishi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la elimu maalum. Naomba Serikali kwanza ibaini idadi ya walemavu tujue kuna walemavu wangapi. Serikali ijielekeze kutoa huduma stahiki za walemavu. Kila mlemavu ana hitaji lake kulingana na aina ya ulemavu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, mlemavu wa ngozi anatakiwa apate mafuta maalum ambayo yatamwezesha kumnusuru na athari za miale ya mwanga. Mlemavu kiziwi, anatakiwa apate shime sikio (earing aid), itakayomwezesha kupata athari za uelekeo wa sauti na mlemavu asiyeona anatakiwa apate fimbo maalum itakayomwezesha kupata uelekeo. Naishauri Serikali, huduma hizi zitolewe bure.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kuwasahau walemavu wa viungo, viungo bandia vimekuwa vikiuzwa kwa bei juu, wananchi wetu hawawezi kumudu. Naiomba Serikali, huduma ya viungo bandia itolewe bure. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naiomba Serikali ianzishe Kurugenzi ya Elimu Maalum. Walimu wanaoshughulikia watoto wenye ulemavu, wanafanya kazi kubwa lakini mpaka sasa hatujakuwa na Kurugenzi ya Elimu Maalum.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu limepakana na Bahari ya Hindi, lina wavuvi, mpaka sasa wavuvi wanatumia mbinu za kijima kuvua. Naiomba Serikali iwezeshe vifaa vya kisasa kwa wavuvi wale ili waweze kwenda kuvua kwenye maji ya kina kirefu na basi kuweza kupata tija.
Katika Jimbo langu la Kilwa Kaskazini, kuna Tarafa mbili ambazo zinalima kilimo cha michungwa. Katika miaka ya hivi karibuni michungwa imepata changamoto ya ugonjwa ambao unakausha mimea hiyo. Naiomba Serikali ituletee wataalam watakaofanya utafiti wa kugundua ni tatizo gani linaloisibu mimea hiyo kukauka ili basi wakulima wetu waweze kupata tija ya zao hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nijielekeze katika utawala bora. Mpaka sasa tunapozungumza, jitihada za kufikia viwango vya juu vya utawala bora bado zinakwamishwa. Bado kuna figisufigisu nyingi katika suala zima la uendeshaji wa utawala bora. Bunge lako Tukufu mpaka sasa linafanya shughuli zake kana kwamba tuko jandoni; kwa sirisiri! Hii nafikiri haipendezi na haiwezi ikawa na mchango mzuri wa ustawi wa demokrasia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado mpaka sasa maslahi na matakwa ya maamuzi ya chaguzi zinazofanywa na wananchi hayaheshimiwi. Kilichotokea Zanzibar ni kutoheshimu matakwa ya maamuzi ya wananchi. Naiomba Serikali izingatie utawala bora ili basi matakwa ya maamuzi
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, ahsante sana.