Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa namna ya pekee kabisa, naomba niwape hongera sana Mawaziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Simbachawene na Mheshimiwa Kairuki na Naibu Waziri, bado ni vijana na mna nguvu, tunataraji mtakimbia na kasi hii na mtafika. Pia kwa namna pekee naomba nimshukuru sana Katibu Mkuu wa Wizara yenu ni mtu msikivu sana, Alhaji Iyombe, kila ukienda ofisini kwake ni mtu wa msaada sana. Alhaji Iyombe kama unanisikia hongera sana kwa utulivu wako na utu uzima wako, endelea kulea vijana hawa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitakuwa na machache ya kuzungumzia. La kwanza ni utawala bora. Wakati Mheshimiwa Bashe anachangia alizungumzia habari ya majizi ambayo yanahama kutoka halmashauri moja kwenda nyingine. Mheshimiwa Waziri Mkuu maadam uko hapa nikukumbushe jambo moja kwamba moja ya majizi makubwa nililokuletea lilipelekwa Nzega kutoka Kasulu.
Mheshimiwa Simbachawene liko tatizo kubwa la wizi uliotokea pale Kasulu wa shilingi bilioni 5.9 kati ya mwaka 2013/2015 na haya majizi bado yanatembea tu na mengine yamehamishwa. Mheshimiwa Waziri Mkuu katika yale majizi yaliyokubuhu, moja ya majizi yale lilitoka Kasulu likaenda Nzega na kule Nzega nimeambiwa amestaafu baada ya kutuibia pesa nyingi sana. Haiwezekani! Huyu mtu lazima atafutwe na afikishwe kwenye mikono ya sheria.
Kwa hiyo, kusema kwamba Nzega ilikuwa ni dumping ground nadhani ni kweli maana hata hilo jizi lililokubuhu lilitoka Kasulu likapelekwa Nzega. Mheshimiwa Waziri Mkuu mtusaidie majitu haya yakamatwe yafikishwe kwenye vyombo vya sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo napenda kulizungumzia alilisema Mheshimiwa Makamba siku anachangia bajeti ya Waziri Mkuu, juu ya utawala bora. Mheshimiwa Simbachawene tuna Halmashauri zaidi ya 34 zinaongozwa na wapinzani wetu kwa maana kwamba baada ya matokeo ya uchaguzi walichaguliwa na wanaziongoza. Nawashauri sana, hizi Halmashauri ambazo zinaongozwa na wapinzani na hizi zinazoongozwa na wana CCM zenye wapinzani wengi vilevile, kuna haja kabisa ya kuzipangia mkakati wa mafunzo maalum vinginevyo hazitatawalika, wataishia kwenye ubishi tu, ndio ni zote, hazitatawalika hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siku ile Mheshimiwa Makamba alisema jambo la msingi kwamba chama cha siasa kikishinda uchaguzi kinaunda Serikali, ni kweli na ndiyo utamaduni wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola. Siyo kuunda Serikali tu, kinaanza kutekeleza ilani yake ya uchaguzi na hakiishii hapo lazima kipate space ya kutawala na wapinzani wetu lazima watupe nafasi ya kutawala, hilo halina ubishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, equally the same, chama tawala nacho lazima kijue kwamba kuna nafasi ya wapinzani katika demokrasia na hiyo space lazima iwepo. Space hiyo Mheshimiwa Simbachawene haiwezi kutoka mbinguni lazima hawa watu wawe trained. Halmashauri 34 zinaongozwa na wapinzani per se lakini ziko nyingine kama 14 hivi zina wapinzani wengi kwa maana kwamba unakuta CCM tumezidi mmoja, wawili, watatu au wanne, kwa sababu ya dhana nzima ya utawala bora lazima kuwe na special program kupitia TAMISEMI kuwajengea uwezo vyama na Halmashauri zote hizi na hasa hizi ambazo zinaongozwa na CCM kwa wingi na hizi ambazo zinaongozwa na wapinzani.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu wa Kambi ya Upinzani niwakumbushe kitu kimoja, opposition maana yake ni kuikumbusha Serikali ya siku isilale usingizi.
Ndiyo utamaduni huo lakini na ninyi kwa sababu mlishindwa uchaguzi mkuu lazima mtoe space ya kutawala kwa watu walioshinda na hilo hatubishani. Mimi sikuwepo siku mbili hizi nimeshukuru sana leo kuona wapinzani wanachangia ndiyo demokrasia hiyo. Ile kukimbia hupati kitu unaposema unatusaidia sisi tujue unachosema, unachofikiri lakini mkikaa kimya mlikuwa mnatunyima haki yetu.
MBUNGE FULANI: Eeeeh.
MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Ndiyo na mlikuwa mnafanya vibaya, lakini sasa nashukuru busara zimeingia, mmewasomesha wameelewa na tutakwenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu ambalo napenda nilizungumzie ni mipango miji. Mheshimiwa Simbachawene unazungumza kwenye hotuba yako upangaji wa miji na kwamba umeisha-identify miji 600, hiyo miji yenyewe iliyopo haina Maafisa wa Ardhi, Maafisa Mipango Miji na haina Valuers. Sasa niulize, hivi kuna tatizo gani la kuajiri moja kwa moja toka kwenye vyuo vyetu vya ardhi wataalam hawa wakaenda kwenye Halmashauri zetu ili kuzuia miji holela? Hili ni jambo muhimu sana, Waziri wa Ardhi uko hapa hebu mshirikiane na TAMISEMI muweze kuondoa tatizo hili. Huwezi kuzungumzia kupanga miji kama huwezi kuwa na wataalam ambao kazi yao ni kupanga miji hii. Jambo hili linawezekana na mnaweza mkalifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la nne ni nyumba za walimu. Nadhani walimu wenzangu mtakubaliana na mimi kwamba kama kuna shida kubwa iliyopo kwenye halmashauri zetu ni nyumba za walimu jamani, walimu hawana nyumba za kukaa, kabisa. Unashangaa sasa kila Halmashauri inakuwa na utaratibu wake wa kuweka kwenye bajeti nyumba 5, 10, 12. Nilikuwa naangalia kwenye kitabu hiki cha TAMISEMI kwenye development, Mheshimiwa Simbachawene una karibu shilingi trilioni moja kwa ajili ya development. Hebu Mheshimiwa Simbachawene hizi fedha za development katika eneo la nyumba za walimu kwa nini ...
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa muda umeisha.
MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana.