Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii muhimu sana. Kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri Kitwanga kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya ndani ya nchi yetu. Tumeziona juhudi zako za kupambana na ujambazi, madawa ya kulevya, kusafisha pale Uhamiaji, Waziri Kitwanga endelea na kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nimekishangaa sana Kiti chako kwa sababu, labda Kanuni zinawezekana zimebadilika. Wenzetu wa upinzani walipewa nafasi ya kutoa maoni ya upinzani. Wameamua wenyewe kwa mapenzi yao, kuondoa hotuba yao mezani. (Kicheko/Makofi/Kelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wale ambao hili Bunge wanalifahamu, hii siyo mara ya kwanza, Wapinzani kuambiwa kutoa maneno wakatoa. Hii siyo mara ya kwanza! Mheshimiwa Tundu Lissu aliwahi kuleta wakati wa bajeti, miaka mitano iliyopita, akaambiwa maneno haya hayafai na kwa sababu ni muungwana akaenda kuyatoa akaja akasoma speech yake. Leo kwa sababu wanayoyasema kwanza hawayaamini, hawana uhakika nayo, ndiyo maana hawawezi kuyatoa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na sisi ngoja tuseme suala la Lugumi.
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti…
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii nimpongeze sana Mwenyekiti wa Kamati ya PAC kwa kazi kubwa anayoifanya. Mambo mengine yalikuwepo huko nyuma, kuanzia mwaka 2011 hakuna aliyeyaona; mwaka 2012, hayakuonekana; 2013 hayakuonekana; 2015 hayakuonekana. Hayakuonekana kwa sababu Kamati hizo waliokuwa wanaongoza wanafahamika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti…
nimepewa na mdogo wangu, kwa bahati mbaya leo naikataa kwa sababu angesubiri nimalize angeweza kunisikiliza vizuri. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Aeshi amefanya kazi kubwa sana kwenye Bunge hili. Amechukua hatua, jambo analifanyia kazi, Kamati zinazunguka nchini kufanya kazi. Sasa leo anapokuja mtu mwingine, anasema amekuja na maswali, ningetamani niyasikie. Maswali hayo, huyu mtu anawahisha shughuli na inawezekana nia yake siyo njema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema nia ni kuisimamia Serikali, Serikali inasimamiwa kwa utaratibu. Wengine inawezekana wamekuja jana ndiyo maana hata heshima ya Kiti hawaijui. Upande wa CCM watu wameongea hakuna watu waliokuwa wanazomea; lakini kwa sababu ya ugeni, mnadhani mkizomea mnafanikiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Aeshi inafanya kazi, tuiache ifanye kazi. Nakuomba Mheshimiwa Waziri, ukiona adui yako anasema anakupenda, ujue huyo ndiyo mbaya wako. Maana kama mtu mmekwenda mmealikana, mmekula chakula, wakati mnaalikana hamkutuambia, lakini mnavyokuja leo mbele ya Bunge hili kusema mliyoyaongea, siyo mapenzi hayo! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri endelea na kazi na bahati njema yote yanayosemwa, kwa namna yoyote ile huhusiki na hili Bunge litasimama kwenye haki. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais Magufuli… (Kicheko/Makofi)
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba unilinde..
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayofanya nchini. Mheshimiwa Rais anarudisha discipline ndani ya nchi yetu, anasimamia mapato ya nchi yetu, kazi hii kubwa anayoifanya siyo wengi wangependa, lazima waumie. Naomba tumpe moyo, aendelee kufanya kazi ili apeleke nchi yetu kule tunakotaka iende. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze Polisi wa nchi yetu. Jeshi la Polisi linafanya kazi kubwa sana. Nchi yetu leo ina amani kwa sababu vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinafanya kazi, vinaheshimika sana duniani. Hakuna jambo la hovyo kama tunavyokutana kama Bunge, tunaanza kukejeli vyombo vyetu vya ulinzi vinavyofanya kazi nchi hii. (Makofi/Kelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza sana watu wa uhamiaji kwa kazi. Leo hii ukiwa unataka kuomba passport utaipata baada ya muda mfupi sana, hili ni jambo jema, naomba liendelee. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia maslahi ya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama yaangaliwe upya ili maslahi yao yaongezwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba niunge mkono hoja. Mheshimiwa Waziri Kitwanga endelea kufanya kazi, Bunge hili linakuamini na tuna hakika utatupeleka tunakotaka kwenda. Naunga mkono hoja hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.