Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa ruhusa yako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni mara ya kwanza nazungumza katika Bunge hili, basi nawapongeza na kuwashukuru Wapiga kura wa Jimbo la Nungwi kwa ujasiri wao wa kulirejesha Jimbo la Nungwi katika mikono ya Chama cha Wananchi CUF na wameielezea dunia kwamba Jimbo haliazimwi, kinachoazimwa ni kiberiti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno hayo, naanza na ukamataji wa Jeshi la Polisi unaoendelea siku hizi, unakuwa hautofautishi baina ya majambazi na Polisi, namna wanavyowakamata raia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, siku ya tarehe 19 mwezi wa Tatu, 2016 ndani ya Jimbo langu katika Shehia ya Kidoti, alikamatwa Mwalimu wa Chuoni, anaitwa Mwalimu Haji Mtumbwi. Mwalimu huyo alifuatwa Chuoni na mtu ambaye kavaa vizuri, hamjuwi kama ni Askari, isipokuwa ni mtu mzuri tu, akamwambia nina shida na wewe tuzungumze. Alipofika kwenye gari ambayo ilikuwa ni ya abiria, ndani anakuta watu wana bunduki na wanamwambia uko chini ya ulinzi na wakamwingiza kwenye gari kwa nguvu pasipo kujulishwa familia yake, pasipo kujulishwa Shehia, pasipo kujulishwa Kituo cha Polisi chochote kilicho karibu. Alipoingizwa ndani ya gari, akafungwa kitambaa cheusi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Polisi wana dhamana ya kulinda usalama na raia wake lakini wanakamata kama hawako katika sheria, wanamchukua mtu kama jambazi, siku tatu hajulikani aliko. Hii ni dhuluma. Jeshi letu la Polisi lisiendelee na mtindo huo. Kama kunatakiwa ushahidi, niko tayari twende na Waziri muda huu huu na mhusika yupo. Hii siyo njia nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nakuja Tumbatu. Tumbatu kumekuwa na mgogoro siku nyingi sana. Tangu uanze Mfumo wa Vyama Vingi 1993 na 1995 uchaguzi wa kwanza, basi kumekuwa na migogoro ambayo inasababishwa na Jeshi la Polisi wenyewe. Kwa sababu 1995 alichukuliwa Ngugu Abbas Ali, wakaingia watu wa CCM wakamkamata wakamchinja kama samaki akapoteza network; kwa hiyo, akachukuliwa akapelekwa hospitali, alipopata fahamu yake akasema kwamba fulani na fulani ndio walionifanya hivi. Mpaka leo hakuna kesi wala hakuna aliyekamatwa. Nani atakuwa anasababisha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 24, mwezi wa Kumi, 2015, siku moja kabla ya Uchaguzi wa tarehe 25 Oktoba, vikosi vya SMZ vilivamia katika Mji wa Jongowe, matokeo yake wakawakamata vijana wanne, wakawakamata wakaenda wakawatesa mpaka wakapoteza fahamu, walipookotwa, kuliko Ulimboka, namna walivyo. Nyang’anyang’a! Ripoti ikapelekwa Polisi Mkokotoni, hakuna hatua iliyochukuliwa. Jeshi la Polisi linashiriki kikamilifu katika kufanya hujuma za kuwaonea wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 29, mwezi wa Kumi, 2015, siku aliyotangazwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. John Pombe Magufuli, sherehe ziliwazidi wana-CCM. Sherehe ziliwazidi wasijifahamu, wakavamia Kijiji cha Kichangani, Tumbatu wakapigapiga watu kwa silaha za kijadi, wakachoma nyumba saba, wakavuruga hali ya amani na utulivu. Matokeo yake, walipokwenda kuweka ripoti hawa waliofanyiwa hivi, wamekamatwa wao na wana kesi wao, kesi namba 116/2015.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijana hawa kumi ambao wamekamatwa na naomba nitaje majina yao Mheshimiwa Waziri uyachukue. Wa kwanza ni Baraka Haji Gora, Faki haji Makame, Haji Abdallah Juma, Haji Sheha Makame, Kombo Makame Kombo, Makame Juma Makame, Musa Haji Omar, Omar Haji Omar, Machano Omar, Faridi Hamis; wamefunguliwa mashtaka wao. Hili ni tatizo kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hujuma hizo kuna mama mmoja amechomewa nyumba yake, yumo ndani moto umeshika hadi juu ya paa.
Anapata tabu hajui pa kukimbilia. Alikimbilia uani. Alipokimbilia uani, akamshuhudia mtu ambaye anachoma, yule fulani.
MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Aaaah… (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante.