Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wajibu wetu wa Kikatiba, Ibara ya 63(2) ni kuishauri na kuisimamia Serikali na Serikali inapaswa isiwe na hofu wakati tunaisimamia na kuishauri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ili kuepuka wizi, ubadhirifu na ufisadi, mikataba yote yenye utata naomba iletwe Bungeni. Kitendo cha Serikali kusema kwamba mikataba ni siri, ni ushahidi tosha kwamba Serikali inataka kuongeza nguvu katika wizi, ubadhirifu na ufisadi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mikataba yote yenye utata ambayo inaashiria wizi, ubadhirifu na ufisadi ni lazima iletwe hapa Bungeni tujue mbivu na mbichi, tuweze kupambanua, tuishauri Serikali tuisimamie Serikali. Mikataba kuwa siri ni tatizo na ndiyo maana tunaunda Kamati siku hadi siku. Hilo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, tatizo kubwa ambalo linaonekana ni namna gani ya udhalilishaji na matatizo ambayo yanawakumba wafuasi hasa wa upinzani kule Zanzibar. Tumekuwa tukisema muda mrefu sana kwamba kunakuwa na hila na njama za kuwadhalilisha Wapinzani Bara na Zanzibar, lakini kule Zanzibar tumeripoti Polisi kuhusu kuchomwa kwa Ofisi ya CUF, Dimani. Sasa ni mwaka mzima hakuna hata taarifa yoyote ya Polisi imesema. Tumeripoti Polisi, Baraza ya Dimani ya Chama cha Wananchi CUF kwamba ilichomwa moto, lakini nasikitika sana Polisi hadi leo hakuna walilojibu. Tumeripoti Polisi Baraza la Kilimahewa, Ofisi ya CUF ya Mjini Magharibi, lakini hadi leo hakuna kitu ambacho kimeonekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijana wetu wa CUF, Chwaka, walikamatwa, wakapigwa na mtoto wa kike akafanyiwa vitendo viovu, tuliripoti Polisi hakuna kilichotokea! Walivamiwa Mpendae kwenye Ofisi yetu ya CUF, wakapigwa, tukaripoti Polisi. Wote wanaopigwa hao ni CUF, tatizo ni nini jamani? Mmeruhusu mfumo wa Vyama vingi ninyi wenyewe! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, haitoshi, kuna wengine wanabambikiziwa kesi. Tuambiwe akina Eddy Riyami, Mansour Yussuf Himid, Naibu Katibu Mkuu Mazuruwi, Hamad Masoud wote hao, lakini tunaambiwa wengine wana kauli za uchochezi, tuseme wanaosema kwamba nchi hii hata ninyi CUF mkishinda, haikupatikana kwa vikaratasi; huo si uchochezi! Tunaambiwa ninyi CUF kama mnataka Serikali Zanzibar, mpindue, hiyo si kauli ya kichochezi! Wanasema kama mnataka Serikali Zanzibar nyie CUF pindueni, huo si uchochezi! Mbona hawa hawakamatwi! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo haya hayakubaliki! Hayakubaliki kwa sababu Polisi inaonekana imeegemea upande mmoja. Tumbatu zimechomwa nyumba nane, Shambuli hana mahali pa kukaa, nyumba 61 zimevunjwa, tumeripoti Polisi, hakuna lolote ambalo limetokea; tatizo nini? Kuwa mpinzani ndiyo tatizo! Huo si uchochezi! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mabango ya Kisonge yote yanaandika siku zote, lakini hii ndiyo hali halisi ilivyo. Tunaomba Polisi, mtuambie sasa, Serikali hii ni ya Chama cha Mapinduzi peke yake au ni ya Watanzania wote na vyama vingine? Hili halikubaliki! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa sana vitendo viovu ambavyo vinafanywa na watu, wanafanyiwa wafuasi wa Chama cha Wananchi CUF na Vyama vya Upinzani, lakini Polisi wananyamaza; hili ni tatizo kubwa!
Mheshimiwa Mwenyekiti, Baraza la Sarayevo, Dimani tuliripoti vizuri na Polisi walituambia tutafanya uchunguzi wa kutosha, upelelezi haujakamilika. Upelelezi mpaka lini? Hawa akina Mansour, Eddy Riyami na wengine wote, tatizo nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana, nimshauri sana Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Ndugu yangu Masauni uwe makini. Hata sisi hapa unapotujibu, unatujibu majibu ya ovyo ovyo ya ufedhuli, ya kiburi na kejeli, ndiyo maana tulikuwa tunakushauri kwamba ni vyema uvae viatu vya Pereira vizuri. Vaa viatu vizuri ili twende vizuri. Vinginevyo sisi tutakuwa hatuendi vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huo ulikuwa ni utangulizi, dakika zenyewe ni tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, NIDA, fedha ambazo zimetengwa hazitoshi, wanazalisha vitambulisho 3,000 kwa siku. Watanzania ambao wanatakiwa wapate vitambulisho hawapungui milioni 25; ina maana kwa hesabu, kila mwaka mmoja…
MWENYEKITI: Ahsante.