Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Waziri wa Habari Mheshimiwa Nape Nnauye kwa hotuba yake nzuri iliyojaa matumaini ya kuona tasnia ya habari ikisonga mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vipaji vingi vya vijana hasa Wilayani hadi Vijijini, lakini vipaji hivi vinapotea bure na vijana kushindwa kuviendeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali hasa hii tasnia ya michezo ifike Wilayani mpaka Vijijini kwenda kuwanoa vijana hawa ili Serikali iweze kuwawezesha na vijana hawa waweze kutimiza ndoto zao. Sio kutimiza ndogo zao tu pia nchi yetu itakuwa ina kiwango kikubwa cha michezo, kwani kuna wakina Samatta wengi huko Wilayani na hasa Wilaya ya Lushoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu shule za habari, utamaduni na michezo. Niishauri Serikali ifungue shule kila Wilaya ili kuibua vipaji vya vijana wetu. Vijana hawa Serikali imewaacha kwa muda mrefu sana hivyo basi katika bajeti ya mwaka huu 2016/2017 itenge pesa kwa ajili ya kuibua fani za vijana hawa pia niishauri Serikali ije iwekeze katika Wilaya ya Lushoto, katika shule ya michezo, Lushoto ni mji ambao una mazingira mazuri, mazingira haya mazuri iliwavutia timu ya Simba na Yanga kuja kufanya mazoezi yao Lushoto.
Pia niishauri Serikali iweze kujenga uwanja wa michezo katika Mji wa Lushoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wasanii katika nchi hii hakuna asiyejua ya kuwa Tanga kuna vipaji vingi vya wasanii. Hivyo niiombe Serikali iweze kuwajengea uwezo wasanii hawa ili nao waweze kufahamika Kitaifa hata Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimuombe Waziri wa Habari na Michezo atenge muda wa kutembelea Lushoto. Mungu ambariki sana Waziri wetu Mheshimiwa Nape Nnauye.