Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kunilinda na kunipa ari ya kuifanya kazi hii muhimu kwa ustawi wa nchi, pia nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuchangia hoja hii.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu unajikita katika kusisitiza utekelezaji wa yale ambayo Wizara imejipangia. Lakini pia kuiomba kutoa kipaumbele kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa wa maji. Mkoa wa Mtwara ni mfano wa maeneo yenye uhitaji mkubwa wa maji, mwaka jana Mheshimiwa Waziri alitembelea na kujionea yeye mwenyewe ambapo maeneo yote bei ya dumu la lita ishirini ilifika shilingi 2,500. Hali hii inajitokeza kila mwaka wakati wa kiangazi.

Naishauri Wizara kwamba Jimbo la Lulindi lina chanzo cha uhakika cha maji cha Mto Ruvuma, hivyo Mradi wa Mbangara - Mchoti naomba uwekewe pesa ya kutosha kwa sasa umepewa shilingi bilioni 1.3 pekee licha ya kuwa ni mradi unaoweza kutatua changamoto ya maji kwa karibu ya nusu ya jimbo; Kata za Lupaso, Lipumburu, Sindano, Mchauru, Mpeta na Chiungutwa na maeneo hayo yako ndani ya kilometa 50 kutoka kwenye chanzo hivyo kuwa ni mradi mkubwa wenye tija unaoweza kutekelezwa kwa gharama ndogo sana.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.