Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, mradi wa maji kutoka Nungwe kwenda Mgodini GGM unatoa maji ghafi katika kata ya Nyamwilolelwa hususani Kijiji cha Kayenze, naiomba Wizara iyatibbu maji haya kabla ya kutumiwa na wananchi. Please establish a treatment plant before human consumption.

Mheshimiwa Spika, mradi unaoendelea wa kuleta maji katika miji midogo ya Katoro na Buselesele toka chanzo cha Chankorongo uongezewe kasi ya utekelezaji, lakini kutokana na ukuaji wa kasi wa miji hii Wizara iongeze pesa katika kupanua mtandao wa maji kila mwaka katika maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Busanda linayo miradi ya visima vya maji iliyo kwenye utekelezaji, niombe itakapokamilika tupate pesa ya mtandao wa maji kwenye vijiji husika.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza RM na DM kwa ushirikiano wao kuhakikisha Jimbo la Busanda wananchi wanakunywa maji safi na salama.