Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia yafuatayo nikianza na sualalal ulinzi na uhifadhi wa vyanzo vya maji. Kuna uharibifu mkubwa wa vyanzo vya maji nchini. Wizara imeweka nguvu nyingi na fedha zaidi kwenye miundombinu na kuliacha suala la uhifadhi wa vyanzo vya maji kwa sekta nyingine hussusan za maliasili. Ni vyema kuanzisha uratibu na miradi ya pamoja na sekta za misitu ili kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji. Tuweke mikakati ya pamoja na sekta za kilimo, mifugo na misitu ili kizitafutia suluhisho la kudumu changamoto zinazotishia uendelevu wa vyanzo vya maji.

Pili ni kuhusu upotevu wa maji; tuongeze fedha zaidi kwa kushirikiana na TAMISEMI ili kukarabati miundombinu ya maji iliyochakaa. Aidha, tuendelee kutoa elimu kwa jamii kujenga tabia ya kutumia maji kwa nidhamu zaidi na kulinda miundombinu yake.

Mheshimiwa Spika, tatu ni kuhusu mabadiliko ya tabianchi sambamba na makazi holela inachangia sana upoteaji wa maji na uharibifu wa vyanzo vya maji. Tufanye kazi kwa karibu na sekta za misitu na ardhi ili kupanga makazi katika hali bora zaidi itakayozingatia uwepo na uendelevu wa vyanzo vya maji. Aidha, tuimarishe dawati la mazingira na mabadiliko ya tabianchi ili kuweza kupata ushauri na kuzingatia athari za mabadiliko ya tabianchi katika shughuli zote za sekta ya maji.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.