Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, napenda kutoa hongera kwa utekelezaji wa majukumu yao na nashauri yafuatayo: -

Kwanza pump kwa ajili ya Mradi wa Kazilankanda, Wilayani Ukerewe ni suluhisho la changamoto ya maji vijijini. Kupitia pesa za UVIKO tulikubaliana na MD RUWASA sehemu ya pesa hizo kununua pump mpya lakini jambo hili limechukua muda mrefu. Naomba pump hii ipatikane mapema kuondoa adha ya maji Ukerewe.

Mheshimiwa Spika, pili ni kuhusu Mradi wa Maji Mjini Nansio, pamoja na jitihada kubwa zinazoendelea, lakini bado wananchi wengi Mjini Nansio hawana maji kutokana na gharama kubwa za kuunganisha maji.

Nashauri Wizara kuikopesha mamlaka iweze kusogeza maji maeneo ya jirani halafu wananchi wakiunganishiwa basi mamlaka iweze kurejesha pesa hizo. Hii itasaidia jamii kupata maji safi na salama.