Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, naomba kwanza kuwapongeza kwa mtiririko na mpangilio mzuri wa hotuba ya bajeti hasa katika viambatisho vinavyoonesha miradi iliyokamilika, inayotekelezwa na ile ambayo itatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, aidha nawashukuru kwamba baada ya mkandarasi wa kwanza wa kuchimba visima katika Vijiji vya Itimbo na Matanana kutokomea, leo kwa maelekezo ya juzi ya Waziri Mheshimiwa Aweso na Katibu Mkuu Engineer Sanga, magari ya kuchimba visima yamewasili leo tarehe 12 Mei, 2022 katika Kijiji cha Matanana na baadae wataenda Itimbo.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha maombi kwenu, kwamba baada ya kuchimba na kwa kurejea mazungumzo yetu kwamba Mafinga as of now ukiacha mradi wa UVIKO katika Kijiji cha Ulole, hakuna mradi ambao unatekelezwa au umetekelezwa. Utakumbuka hata Mradi wa Vijiji vya Ugute na Ulete wanasema vilikuwa vimesahaulika, mmetumia neno oversight. Kwa sababu hiyo, naomba mtusaidie baada ya kuchimba visima hivi vya Matanana na Itimbo, design ifuatie ili tukamilishe katika mwaka wa fedha 2022/2023. Kwa kifupi ninaomba mradi au mwendelezo uingie katika bajeti hii tunayoipitisha sasa. Mkitusaidia maana yake tutakuwa tumemaliza vijiji hivi kwa ukamilifu.

Mheshimiwa Spika, suala la pili; baada ya mazungumzo yetu katika Kikao (Mheshimiwa Aweso, Mheshimiwa Chumi, Katibu Mkuu - Engineer Sanga, Ndugu Bwire na RM Joyce), nilifahamishwa kwamba kwa kuwa kulikuwa na oversight Wizara iko katika hatua mwisho kutangaza na jana nashukuru sana kupitia Ndugu Bwire nimefahamishwa kuwa tangazo la tender tayari. Hata hivyo, katika kitabu chenu vijiji hivi viwili vya Ugute na Ulete havipo, ninapata shaka kuwa isije ikafika wakati wa utekelezaji ikaonekana vijiji havipo katika kitabu cha bajeti, hivyo nashauri izingatiwe ili vijiji hivi ambavyo kimsingi ni mwendelezo wa miradi ya mwaka huu wa fedha wa 2021/ 2022 viweze kuwa reflected kwenye kitabu cha bajeti ya mwaka 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, ombi la gari; nafahamu kwamba kuna uhaba mkubwa wa magari, hata hivyo ninaomba kwa jicho la kipekee, mtusaidie kupata gari la uhakika ambalo litaweza kusaidia RUWASA na MAUWASA, kwa sasa gari la RUWASA Mufindi ni kuukuu na MAUWASA hakuna gari kabisa. Kwa kasi ya ukuaji wa Mji wa Mafinga ikiwa ni pamoja na viwanda vya mazao ya misitu na vijiji vinavyozunguka, upo umuhimu mkubwa sana kutusaidia kupata gari.

Mheshimiwa Spika, mwisho, kwa dhati ya moyo wangu nawapongeza sana kwa namna ambavyo miradi inafuatiliwa kwa ukaribu na ushirikishwaji sisi Wabunge, walau sasa miradi inafanyika kwa speed, naamini hata Mradi wa Miji 28 utatekelezwa kwa speed na ufanisi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.