Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwapongeza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Anastazia Wambura respectively. Naipongeza timu yote ya wanahabari hususani TBC, TBC Taifa na wengine wote wa Wizara hii. Nimpongeze pia Dkt. Elisante, mwalimu wangu wa siku moja, I hope nitaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mdogo, pamoja na kazi nzuri wanazozifanya TBC na TBC Taifa, nashauri kuanzishwe kipindi maalum kama kilivyo kile cha Bango au Chereko, kipindi hicho kiwe cha aidha Mbunge wangu au Jimbo langu au Nimetimiza Ahadi Yangu. Kipindi hiki kiwe cha kulipia badala ya kupata nafasi kwa kubahatisha na pia bure kabisa. Ni vema tuchangie hata kama shilingi 200,000 kwa dakika 30 au hata kama ni kwa dakika 15. Kipindi hicho kituwezeshe Wabunge kuzungumzia utekelezaji wa kazi zetu au kuwapasha habari wananchi wetu. Pamoja na kuchangia bado isiruhusiwe mtu kusema vyovyote anavyotaka, ethics lazima iwe observed. Fedha hizo zitasaidia kupunguza kero ndogo ndogo za wanahabari wetu.