Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Waziri, Naibu Waziri pamoja na watendaji wote wa Wizara kwa kuwasilisha bajeti hapa Bungeni ili tuweze kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo ambayo nilikuwa naleta ili kupatiwa ufafanuzi na kutoa ushauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu viwanja vilivyojengwa kwa ajili ya michezo, naomba Serikali inipatie majibu kuhusu viwanja vilivyotengwa kwa ajili ya michezo na Halmashauri zetu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja hivi watendaji wa Halmashauri waliamua kuvigawa na vikafanyiwa uvamizi yakajengwa majengo na baadaye Serikali ikatoa tamko kuwa wavamizi na maeneo ya wazi yaliyotunzwa kwa ajili ya michezo wabomoe lakini tamko hilo halijatekelezeka mpaka leo. Na kila siku tumekuwa tukiuliza maswali kuhusiana na jambo hilo lakini yanajibiwa kisiasa zaidi. Sasa naomba kujua jambo hili, Serikali imelichukulia vipi kwa sababu hatuwatendei haki vijana wetu, vipaji tunavitengenezea vipi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba kujua sheria za vyombo vya habari ni lini italetwa hapa Bungeni, kwa sababu tunaamini kuwa sheria hii ndiyo muarobaini wa matatizo yote katika vyombo vya habari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu michezo ya UMISETA na UMISHUMTA. Michezo hii kwa sasa haina ari kabisa, ni imani yangu kama Serikali ingeamua kuwekeza mikono katika shule za msingi na sekondari zingeweza kuibua vipaji na tungeimarisha michezo yetu hapa nchini na kupata wachezaji bora. Inasikitisha kuona kuwa michezo ya shule za sekondari na msingi inapoanza shule nyingi watembeze mabakuli ya kuomba omba vifaa vya michezo mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Tanzania tutakuwa na Vazi letu la Taifa?. Serikali imekuwa kila mara ikitupatia taarifa kuwa Vazi la Taifa lipo katika mchakato. Ifike wakati tuambiwe kama imeshindikana tuambiwe ili tusiendelee kusubiri jambo lisilo na mwisho. Ni fahari kubwa kutambulika kwa mavazi kama zilivyo nchi nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali bado haiwezi kutoa kipaumbele timu ya wanawake, mbona timu ya Taifa inatafutiwa mpaka kocha wa kigeni kwa nini timu ya Twiga bado mpaka leo wanatembeza bakuli tu wanapokuwa na mashindano? Ni lini watapewa fungu au kutengewa katika Bajeti ya Serikali? Naunga mkono hoja.