Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii nzuri ya kuchangia bajeti ya Wizara ya Maji. Awali ya yote nimshukuru sana Rais kwa namna ya pekee kabisa kwa jinsi ambavyo anapambana kuhakikisha Watanzania wanapata maji. Hii inatokana na a very strong political will aliyonayo pamoja na ubunifu mkubwa alionao katika kutafuta fedha.

Mheshimiwa Spika, pia pale Serengeti tuna watu wa RUWASA wanafanya kazi nzuri sana wakiongozwa na Eng. Mchele. Wameendelea kupambana kila wakati kuhakikisha mambo yanaenda vizuri. Tunao watu wa MUGUWASA, taasisi inayosimamia utoaji wa maji katika mji wa Mugumu, pia wanafanya vizuri sana, na hivi karibuni kulikuwa na shida kubwa ya maji kuchafuka kutokana na tope la mvua nyingi kunyesha bado walifanya vizuri wakasafisha matenki, kwa hiyo wanafanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, ombi langu kubwa kwa taasisi hizi mbili ni kwamba taasisi hizi ziongezewe vifaa vya kutendea kazi. Watu wa RUWASA hawana gari za kutosha, wanayo gari moja na imechoka ilhali wana miradi mingi ya kuisimamia. Kwa hiyo niombe sana Wizara, nimeona kwenye bajeti hamjawawekea fedha kwa ajili ya gari, niombe muwafikirie kuwaongezea gari. Lakini pia wanao watumishi wachache. Kwa mfano RUWASA wanaye engineer mmoja tu, engineer Mchele ambaye yeye huyo huyo ndiye Mkuu wa RUWASA katika wilaya nzima. Kwa hiyo mostly anafanya kazi za administration. Kwa hiyo tuongezee watumishi ili waweze kusimamia miradi hii vizuri kwa sababu component ya usimamizi ni ya muhimu sana ili tuweze kuwa na miradi mizuri na inayokamilika vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia nitumie nafasi hii kuwapongeza sana Wizara hii ya Maji. Wizara hii mnafanya vizuri sana, tumeona mkisimamia na kutekeleza majukumu yenu kwa umahiri mkubwa. Hii imechangia Wizara hii kuwa na mafanikio makubwa sana. Kipekee sana nimshukuru Rais wetu kwa kutupatia kijana makini mahiri kabisa, rafiki yetu Aweso, anafanyakazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Baraza kuwa limetangazwa Waziri wa kwanza kukutana naye nilikutana na Aweso. Aweso ni mtu mahiri, ni msomi mzuri lakini ni mtu yuko tayari wakati wowote kupokea mawazo ya na maoni ya watu. Ni mtu unayeweza pia ukamkosoa, hana tatizo anasikiliza na anapokea mambo. Kwa hiyo nilizungumza naye na kukosoa jinsi utekelezaji wa mradi wa chujio pale Mugumu ulivyokuwa ukiendelea; na Awezo aliniambia hebu usiwe na wasiwasi hii umetoboa. Kweli baada ya muda mfupi niliona utekelezaji mkubwa fedha imepatikana na mradi ule ukakamilika; kwa hiyo tunashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, lakini kuna jambo moja ambalo katika bajeti iliyopita, hii tunayoenda kukamilisha, ya mwaka 2021/2022; niombe sana Wizara, tuliomba kiasi cha milioni 800 hii ilikuwa kwa ajili ya kuhakikisha mradi huu sasa unapanuka kiasi cha kutosha. Kwa kufanya hivi ingetuwezesha kuondoa utegemezi ambao upo. Kumekuwa na utegemezi sana katika kuendesha ule mradi na kila mara tunawapigia simu umeme unakatwa kwa sababu mradi ule hauwezi kulipa gharama za umeme na zingine na zingine, sasa imekuwa ni shida. Pamoja na kazi hii nzuri ambayo Serikali imefanya ya kutupatia fedha na mradi ule wa chujio kukamilika na expansion ile ambayo Mheshimiwa Aweso ulipokuja mwisho wa mwaka wa jana ukatuongezea milioni 527; expansion ya mradi ule umefanyika kuelekea katika tenki ni nzuri lakini maji mara kwa mara yanakatwa. Sisi tuliamini kwamba kwa kupata hii milioni 800 tutapanua wigo wa mradi ule ili watu wengi wapate maji ili katika multiplier effect tunaweza tukapata fedha nyingi za kuendelea kuendesha ule mradi sisi wenyewe.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tuombe sana katika muda huu uliobaki mtusaidie fedha hizi ili tuweze kukamilisha mradi ule na tuweze kusimama imara na kuendesha huu mradi vizuri. Hii itaondoa manung’uniko ya wananchi ambayo yanakuwepo mara kwa mara hasa huduma ya maji inapokatwa.

Mheshimiwa Spika, lakini pia ni vizuri ikakumbukwa kuwa mradi huu pamoja na kwamba kuna mradi ule wa miji 24, 28 bado ni muhimu kuendelea kupanua mradi huu, ambapo tayari tutakuwa tumeanza kufanya kazi ya sehemu ya mradi ule mkubwa unaokuja. Kwa hiyo tunaomba hili tuweze kutekelezewa.

Mheshimiwa Spika, lakini tunashukuru sana, kuna miradi mingine ambayo imeweza kukamilika katika baadhi ya vijiji kule Robanda kuna miradi mingine Makundusi kule Kebancha na vijiji vingine vingi. Tunaona kuna miradi inaendelea katika vijiji 56. Kwa kweli ni commitment kubwa na fedha hii imetolewa lakini bado pamoja na miradi hii mingi inayoendelea bado kuna zaidi ya vijiji 24 ambavyo bado havina maji kabisa. Kuna vijiji vya Masinki, Magange kuna vijiji vya Nyamihuru kuna ukienda vijiji vya kule Bisalala kuna vijiji vya Robanda ambapo tayari tumepata kisima kimoja lakini bado sehemu ni kubwa sana ambayo inahitaji maji.

Mheshimiwa Spika, bado ukienda Bwitengi na vijiji vingine vingi kama vile Kebosongo vingi sana havina maji. Sasa katika ile 85% ambayo Wizara imekusudia kufikia by 2025 naona Serengeti tunaweza tuka-lag behind, kwa hiyo tuwaombe sana Wizara tuone kila linalowezekana katika bajeti, hii kuona kwamba mmetutengea bilioni nne point something bado kungehitajika fedha nyingi zaidi ya kuongeza maana naona pale kuna vijiji kama vitano ambavyo vimewekewa fedha ambavyo ni Vijiji vya ijiji Ligicha, Nyiberekera Singisi pamoja na Nyamisingisi ambavyo viko jirani ambavyo mngeweza mkavi-connect na hiyo project havina maji bado.

Mheshimiwa Spika, lakini pia niombe katika bajeti hii mpya 2022/2023 kuna mradi ule wa miji 28. Pale Serengeti tunahitaji mradi ule uweze kuwa mkubwa zaidi. Lile bwawa la Manchila wakati linajengwa lilikuwa kwa ajili ya kutafuta temporary solution ya maji katika mji wa Mugumu ambao ni Makao Makuu ya wilaya. Wakati ule Mugumu ilikuwa ni kijiji ilikuwa na watu wachache sasa watu ni wengi na ule mji bado unaendelea kuwa mkubwa; na hivi karibuni tunaendelea na maandalizi tukishirikiana na Serikali ya wilaya kwenda kwenye project kubwa sana ya Smart City.

Mheshimiwa Spika, project hii inaenda kujenga itahusisha ujenzi wa mahoteli makubwa kwa ajili ya huduma za kitalii tunaenda kujenga miundombinu mikubwa facilities nyingi sana ambazo zinahitaji maji. Maji katika lile bwawa ni lina cover kama ni almost mita cubic milioni 14.2 na wataalamu wanaonesha miaka 15 hadi 20 ijayo litashuka mpaka kufikia mita cubic 6,000,000 sasa hii na mategemeo yetu kwa miaka 10, 20 ijayo tunaweza tukawa tunahitaji zaidi ya mita cubic milioni 30.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kuna haja sasa huu mradi mkubwa badala ya kutumia bwawa la Manchila sasa mwende kuu-connect na ule mradi mkubwa unaotoka Mugango – Kyabakari – Butiama. Kutoka Butiama mpaka Mji wa Mugumu ni kilomita 90 tu. Tukifanya hivi tutapata maji ya kutosha na maji kwa muda mrefu. Ni vizuri tukafikiria kuwa na solution kuwa na matatizo ya muda mrefu kuliko kila siku ku-invest katika mean solution za muda mfupi, baada ya kusema haya naunga mkono hoja ahsante.