Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, nianze kuipongeza Serikali ya CCM kwa kazi kubwa na nzuri inayofanywa katika sekta ya elimu, pia nampongeza Mheshimiwa Rais, Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa anazozifanya kwenye sekta ya elimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali imejenga madarasa mengi sana nchi nzima na kwa mara ya kwanza Tanzania imebadilisha historia kwa wanafunzi wote waliofaulu kupata nafasi ya kuingia kidato cha kwanza. Ongezeko la madarasa haya imeongeza idadi ya upungufu wa walimu. Naishauri Serikali iongeze ajira za walimu ili idadi ya madarasa iendane na idadi ya walimu.

Mheshimiwa Spika, changamoto nyingine ni shule za zamani kuwa na uchakavu mkubwa, naishauri Serikali pia ifanye ukarabati wa shule hizo kongwe ili ziendane na shule mpya zilizojengwa sasa hivi. Sambamba na hilo ipo changamoto ya walimu kukosa nyumba karibu na shule wanazofundishia, niendelee kuishauri Serikali ijenge nyumba za walimu kupunguza changamoto hiyo.

Mheshimiwa Spika, niongelee kuhusu mitaala yetu ya elimu, nashauri Serikali kuwa mitaala yetu iendane na mafunzo ya ufundi iwe kuanzia darasa la kwanza kumwezesha mwanafunzi anapomaliza shule awe anaajirika na awe na uwezo wa kufanya kazi na awe anaweza kujiajiri.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.