Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Spika, kwa miaka mingi kumekuwa na changamoto nyingi sana kwenye suala la elimu nchini hasa katika vitendea kazi katika ufundishaji wa michepuo ya sayansi. Natoa rai kwa Serikali kutatua changamoto hii na kuweka vifaa vya laboratories katika shule za sekondari. Walimu wana changamoto kubwa sana mashuleni hasa kulingana na Serikali kutoajiri walimu kwa muda mrefu hii inafanya walimu kuelemewa mwalimu mmoja anafundisha madarasa matano. Tunaomba Serikali iaajiri walimu wapya ili wapunguze mzigo mkubwa wa vipindi kwa walimu wachache ambao hawakidhi mahitaji ukilinganisha na idadi ya wanafunzi.

Tunaomba Serikali iendelee kuwalipa walimu stahiki zao, wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu. Walimu wamekuwa na hali ngumu hasa wale wanaopangiwa shule za vijijini. Tunaomba Serikali iendelee kuwawekea mazingira bora walimu ili wafanye kazi zao kwa ufanisi.