Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, naungana na Watanzania wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa majaliwa yake katika Taifa letu kwa jinsi alivyotuvusha kupitia changamoto mbalimbali kama vile janga la Corona, mafuriko, mioto, ajali mbalimbali na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wetu mpendwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi anavyoiongoza nchi yetu na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Profesa Mkenda, Waziri wa Wizara hii; Mheshimiwa Omary Kipanga - Naibu Waziri wa Wizara hii; pia nampongeza Mheshimiwa Sodoyeka Katibu Mkuu wa Wizara hii; Naibu Makatibu Wakuu wa Wizara hii; Wakurugenzi na watendaji wote wa Wizara hii kwa jinsi mnavyoitumikia Wizara hii hongereni sana Mwenyezi Mungu awabariki sana.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nitoe mchango wangu kupitia hotuba ya mapendekezo ya Wizara hii muhimu sana kwa ustawi wa Taifa letu; kwanza naipongeza sana Wizara kwa mpango wake wa kufanya mapitio ya sera yetu ya elimu ili kuendana na mahitaji muhimu kwa wakati uliopo na ujao, na mchakato wa kuchukua maoni ya wadau mbalimbali kuhusu mtaala wa elimu yetu ili kumwezesha Mtanzania kukabiliana na mazingira ya karne ijayo katika dunia hii.

Mheshimiwa Spika, Serikali itusaidie kuanzisha Kitengo cha Elimu Maalum kila halmashauri kwenye shule moja ya msingi katika tarafa ambayo iko katikati ya kila halmashauri mfano huo uko kwenye Halmashauri ya Mji wa Mbulu Shile ya Msingi Endagikort ambayo ina wanafunzi zaidi ya 30.

Mheshimiwa Spika, napongeza pia hatua ya Wizara kumtuma Mkurugenzi wa Elimu Maalum Dkt. Matonya kuitembelea Shule ya Msingi Endagikort, asanteni sana.

Ninaomba Wizara itusaidie kurasimisha kitengo hicho na kujenga bweni la kulala wanafunzi wa elimu maalum. Hivyo basi wakati tukielekea huko tusisahau kuona elimu ya vyuo vya ujuzi hasa vyuo VETA na FDCs mitaala yake kufanyiwa mapitio ili kumwezesha mhitimu kufika chuo kikuu kwa ngazi za kuhitimu secondary school, cheti cha ufundi, diploma hadi shahada.

Mheshimiwa Spika, kwa moyo wa dhati ninaiomba sana Serikali itoe fedha za awamu ya pili kukamilisha ujenzi na ukarabati wa majengo ya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi - Tango FDC Mbulu kwa kuwa ujenzi wa awamu ya pili ulishakamilika kwa kiwango cha juu sana, kwani Tango FDC ilijengwa miaka 60 iliyopita hivyo majengo mengi ni chakavu sana na hatarishi kwa matumizi.

Mheshimiwa Spika, kwenye mitaala ya elimu ya msingi na sekondari tusisahau kuingiza masomo ya maarifa ya jamii, kilimo, mifugo, biashara kwani zaidi ya 50% ya vjana wetu wahitimu wa kidato cha nne ndiyo Watanzania wa kawaida ambao hawataweza kwenda kwenye elimu ya juu kwa hiyo, maarifa na ujuzi watakayopata kwa ngazi hizo za msingi na sekondari inayowaweka kwenye hali ya kukabiliana na changamoto za kukabiliana na maisha ya kawaida.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja 100%.