Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshiiwa Spika, kwa kuwa vyuo vipya vya VETA kikiwemo cha Ukerewe vinaelekea kukamilika, nashauri yafuatayo; kufanyike maandalizi ya vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia ikiambatana na mafunzo kwa walimu na wakufunzi wa vyuo hivi ili waweze kutoa elimu inayoendana na mabadiliko ya kiteknolojia na hivyo kutoa mazao yenye uelewa wa teknolojia ya sasa na hivyo kuwa rahisi kushiriki kwenye mapinduzi ya uchumi kwenye Taifa letu.

Kuhusu mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ualimu cha Murutunguru bado haujakamilika kutokana na fedha kutokupelekwa. Kutokana na umuhimu wa chuo hiki katika kuzalisha walimu kwa ajili ya kufundisha vijana wetu, nashauri fedha zipelekwe ili mradi huu uweze kukamilika na kutoa huduma iliyotarajiwa.

Katika Wilaya ya Ukerewe, kuna ongezeko kubwa sana la watoto na hivyo kuwa na mrundikano mkubwa wa watoto mashuleni, nashauri kuwe na programu maalum ya kufanya tathmini na zijengwe shule nyingine mpya au shikizi na zipewe raslimali pesa pea za kutosha kuwezesha program hii. Kwanza, kidato cha nne baada ya kuhtimu, waliofaulu waanze kidato cha tano mapema.

Kutokana na maendeleo ya TEHAMA na masuala mazima ya IT, matokeo ya kidato cha nne yamekuwa yakitoka mapema, Kuna wakati by January/ February matokeo yanakuwa yameshatoka. Hata hivyo kwa mujibu wa kalenda ya kitaaluma, wanafunzi hawa hulazimika kukaa almost miezi mitano idle. Kwa kuwa siku hizi wanafunzi wanamaliza mapema sana, wapo watoto wanamaliza wakiwa na miaka 15 umri ambao ni risk sana mtoto kukaa idle miezi mitano. Nashauri tuone uwezekano wa wanafunzi hao wanaomaliza na kufanya kidato cha nne mwezi Novemba, waanze masomo ya kidato cha tano mapema mwezi Machi walau kupunguza muda wa kukaa idle nyumbani. Aidha, pawepo na link kati ya Wizara ya Elimu/ TCU na Wizara ya Utumishi/Sekretarieti ya Ajira.

Katika miaka ya karibuni vyuo vimekuwa vikibuni course ambazo ni mpya ili kuendana na mahitaji. Hata hivyo inaonekana kuwa ni kama hakuna mawasiliano kuwezesha course hizo mpya kutambulika katika mifumo ya ajira. Kwa mfano hivi karibuni TRA ilitangaza kazi kupitia Sekretarieti ya Ajira lakini baadhi ya applicants wameshindwa ku-apply kwa sababu tu course hiyo haitambuliki.

Kwa mfano course hii; Development Finance& Investment Planning inayotolewa na Chuo cha Mipango, ndani ya course hii wanafunzi wanasoma course ambazo zinafundishwa pia IFM kama vile Public Finance And Taxation, Accounting, International Finance, Cost Accounting na kadhalika, hata hivyo mwaka 2020 wanafunzi wa course hii mfumo haukuwatambua katika nafasi zilizotangazwa za Tax Management na nafasi Customs Management. Huu ni mfano mmoja halisi ambao mnaweza kujiridhisha katika Chuo cha Mipango Dodoma.

Ushauri; nashauri Serikali ishirikiane kuzitambua course na kuziingiza katika sifa/mifumo ya ajira, ndio maana nasema pawepo na link kati ya Wizara/TCU na Utumishi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.