Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kuwapongeza kwa kuimarisha suala la udhibiti ubora kwa kutoa mafunzo kwa Walimu na Maafisa Elimu Kata, kwa sababu ubora wa elimu yetu hasa kuanzia ngazi ya msingi na sekondari ni jambo muhimu sana.

Pili ni kuhusu elimu jumuishi; napongeza hatua zinazochukuliwa na pia shukrani kwa Wizara kuisaidia Shule ya Msingi Mchanganyiko/Jumuishi ya Makalala ambayo iko katika Halmashauri ya Mafinga Mji, mazingira ya shule hii sasa yanavutia na pia kupitia wahisani wa Water for Africa, shule imepata kisima kirefu na kufungiwa mfumo wa maji ya moto. Nawashukuru sana.

Hata hivyo, ninawasilisha maombi ya gari kwa ajili ya shule hii ambayo ipo umbali wa kama kilometa tano kutoka Mafinga Mjini. Hii ni kwa sababu shule hii inahudumia watoto wenye ulemavu wa akili, wenye uono hafifu na wenye ualbino ambao wengi wao familia zao zimewatekeleza kiasi kwamba hata shule ikifungwa watoto wanabaki shuleni. Aidha, watoto hawa wakiugua inawapa walezi wakati mgumu kuwahudumia kwa sababu hospitali iko umbali wa kama kilometa saba. Kwa ufupi naomba mtusaidie kuitazama shule hii kwa macho mawili kwa sababu pia inahudumia watoto kutoka nje ya Mafinga, kwa mfano kuna watoto kutoka Makambako (Njombe) na Rujewa (Mbeya).

Mheshimiwa Spika, shukrani kwa Shule ya Sekondari ya Nyamala kupata kibali na kupokelewa kuwa shule ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mafinga Mji ilinunua Shule ya Sekondari ya Nyamalala ambayo ilikuwa shule binafsi. Tuliwasiliana na Ofisi ya Waziri na kupata usaidizi wa haraka na ushirikiano mkubwa na kukubaliwa ombi letu la shule hii kuwa ya Serikali. Pamoja na shukrani hizi naomba kukumbusha ili iingie katika mipango ya mwaka ujao wa fedha wa 2022/2023. Nafahamu kuwa shule hizi zinasimamiwa na TAMISEMI, hata hivyo kwa yale ambayo yako chini ya Wizara ya Elimu basi naomba ikumbukwe. N5aomba kuwasilisha.