Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi mwenye Enzi na Utukufu kwa nafasi hii ya kusimama mahala hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nami nichukue nafasi hii pia kuwapongeza sana Mawaziri wa Wizara hii ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mawaziri wengine waliopita katika Wizara hii kwa hatua mbalimbali ambazo wanazichukua katika kuhakikisha kwamba taifa letu linakwenda kwenye elimu ambayo ina-respond to the middle of the time and society.

Mheshimiwa Naibu Spika ukisikiliza michango ya Wabunge wote ambao wamechangia tangu jana, hakika tunahitaji kama taifa kuwa na elimu ambayo ina-respond to the need of the time and society. Mheshimiwa Kishimba amekuwa akitoa mifano ambayo inaonekana kama mifano ya utani utani, lakini kiuhalisia ni kwamba tunahitaji elimu ambayo ina- respond to the need of the time and society. Maana ya kusema hivi ni nini, ni kwamba ni wakati sahihi kama taifa sasa tuendelee ku-enhance katika practical science.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na vyuo vyetu ambavyo vinatoa elimu mbalimba za kiufundi. Kwa mfano labda tumekuwa tunasoma labda mechanical engineering, lakini kwenye mechanical engineering utakuta unafundishwa zaidi namna ya ku-resolve forces katika mifumo ile ambayo inaendesha mitambo ule badala ya kufundishwa pia na production. Kwa hiyo mimi nishauri, nishauri sana, badala ya kuwa Department ya Mechanical Engineering kama kweli tunataka kwenda kwenye Industry na elimu ambayo ina meet the need of time and society, tulipaswa kuwa na Mechanical Engineering and Production ili tuweze kutengeneza mind set ya production katika mifumo ya uzalishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu wametangulia kusema hapa kwamba lengo namba nne la Maendeleo Endelevu la Dunia ni Elimu. Lakini naomba niseme kwamba lengo lile linazungumzia quality education, lakini uhalisia nchini kwetu tuna inequality in acquiring education. Hakuna usawa nchini katika kupata elimu. Kwa nini nasema hivi; sote sisi ni mashahidi kwamba elimu tuliyonayo wala si ya kwetu tumefanya kuletewa na wakoloni. Mkoloni A aliingia Mkoa A, Mkoloni B aliingia Mkoa B na Mkoloni C aliingia Mikoa C. Tumeona hapa Curriculum au Mtaala wa Kwanza ulikuwa wa Ujerumani na Mtaala wa Pili wa Elimu ulikuwa wa Mwiingereza, lakini hatujawahi kusikia Mtaala wa Tatu wa Elimu ulikuwa ni wa Mwarabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nikizungumza hivi nazungumza kulenga kwamba hakuna usawa katika upatikanaji wa Elimu nchini Tanzania kwa sababu kuna mikoa bado ipo nyuma kielimu. Mikoa hii iko nyuma kielimu si kwa kutaka kwao. Kama ambavyo vilevile naweza nikasema Adolf Mkenda hakutaka kuzaliwa Kilimanjaro kama ambavyo Chikota hakuta kuzaliwa Mtwara; imetoka tu by chance. Vivyo hivyo Adolf Mkenda hakutaka Mjerumani aende Kilimanjaro bali ilitokea tu by chance. Kwa hiyo mimi nataka kusema kama nchi wakati tunafikiria kwenda kwenye quality education vilevile tufikirie kwenda kwenye equality in acquiring education. Kwa mujibu wa sustainable development goals tunasema kwamba no one should be left behind in stantiable development. Kwa hiyo kama hakuna equality kwenye education inamaana kuna watu bado wataendelea kubaki nyuma katika maendeleo endelevu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tafiti zinaonesha kwamba, mzazi ambaye hakufika au hakupata elimu ni ngumu mtoto wake kufika elimu ya juu. Tafiti pia zinaonesha kwamba, ili tuweze ku-brake poverty circle elimu ni factor muhimu sana. Nini nataka kusema, inamaana katika taifa hili bado kuna Mikoa itaendelea kuwa kwenye absolute poverty na wengine wataendelea kuwa hivyo kwa mujibu tu wa ukoloni ambao umetuletea elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi ninaomba kama taifa, wakati tunakwenda kutengeneza au tunakwenda kufanya mapitio ya Sera ya Elimu vilevile tufanye tafiti ya kujua ni kwa nini baadhi ya mikoa nchini Tanzania iko nyuma kielimu. Na tuje na recommendations ambazo zitaweza kusaidia mikoa ile kuinuka kielimu bila kuathiri ambao wameshaendelea kielimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, na maana yangu ya kusema hivi ni nini, inawezekana tunapeleka resources mahala ambako hakuhitajiki resources hizo. Namaanisha kwamba inawezekana kuna mahala tunahitajika kuongeza nguvu za mind set and transformation change lakini tunapeleka mavitu ambayo mengine hayahitajiki. Kwa hiyo kama Taifa ninaomba sana tufanye tafiti kuja kujua ni kwa nini baadhi ya maeneo yako nyuma kielimu nchini Tanzania na maeneo mengine yako mbele kielimu na tuje na recommendations ambazo zitakazotuwezesha kutengeneza mtaala utakao-meet u-meet the need of the time and society.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile, kama taifa letu tunapaswa pia Elimu i-align na mipango mingine ya taifa hili. Nimejaribu kupitia Hotuba ya Mheshimiwa Waziri, ile item 2114 ya Usimamizi wa Elimu Maalum; na kuna utekelezaji kadhaa pale ambao umefanyika. Hata hivyo kiuhalisia bado inaonekana kwenye elimu maalum tuko nyuma ya wakati. Tumeshindwa ku-align na mipango mingine ya taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye elimu maalum kuna haja ya kuzalisha walimu wa speech therapy ili kwenda sawa na mipango ya Wizara nyingine za taifa letu. Serikali imeshatumia billions of money wamepeleka watoto India kwenda kupandikiza usikivu, lakini wanaporudi nchini watoto wale hakuna mahala ambako wanawekwa ili ku-develop speech. Hakuna madarasa ambayo yameingizwa katika elimu maalum ili watoto wale waweze ku-develop speech na walimu...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante, kengele ya pili. Ahsante kwa mchango mzuri.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: …kama Taifa tuone namna ya ku-align mipango yetu na mipango ya elimu pamoja na mipango mingine ili watoto wetu waweze kupata kile ambacho kinahitajika kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Naunga mkono hoja.