Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami kuwa mchangiaji wa mwanzo katika Wizara hii ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia. Nawashukuru sana Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yake kwa maana ya bajeti yao nzuri, kwa namna walivyoweza kuwasilisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda sana kuchangia katika maeneo mawili ambayo kwangu nadhani wanapaswa kuya-consider. Ukiangalia hii Wizara ya Elimu, maana yake ni kwamba hao ndio wanaoanza kuwandaa vijana wafike mahali waanze maisha. Kwa hiyo, kwa namna yoyote ile katika haya maandalizi yao lazima wawe wameangalia zaidi kwamba mwisho wale vijana wakimaliza shule wanahitaji wapate ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kusema kweli katika nchi yetu hapo ni kati ya mahali ambapo tuna tatizo kubwa, kwamba vijana wengi wanamaliza shule na wanahitaji waajiriwe ili waendeleze maisha yao. Kwa bahati mbaya sana na hata ukiangalia katika nafasi ambazo zinatokea, wanaopata nafasi ni wachache lakini wanaomaliza shule ni wengi zaidi. Kwa hiyo, nilidhani kwamba ninyi kwa sababu ndio waandaaji wa sera na miongozo, ni vizuri mngejikita sana kuangalia namna gani wale vijana wanaomaliza shule wataweza kupata ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, leo ukiniuliza kwenye elimu hasa ya Chuo Kikuu ambapo sasa hivi ndipo mmeangalia sana, pamoja na ile elimu ya vyuo vya kati, hebu tujitahidi kuweka nguvu kubwa katika vyuo vya kati. Ni ukweli usiopingika kwamba leo ukimchukua kijana, mfano aliyemaliza Chuo cha VETA, halafu ukamchukua mwingine ambaye amemaliza Political Science Chuo Kikuu, ukiwapeleka duniani, yule mwenye elimu ya certificate anaweza kuendesha maisha yake kushinda yule wa Chuo Kikuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo ni kwa sababu ukienda kwenye hivi vyuo vya kati, wanafunzi wengi wanajifunza moja kwa moja yale maisha ya kawaida. Mfano, ufundi makenika, ufundi wa magari, useremala pamoja na fani mbalimbali. Kwa hiyo, nilidhani kwamba pamoja na hizo juhudi za Serikali kuviangalia hivi vyuo vya kati, ingeweka hapo nguvu zaidi kuliko inavyoangalia sasa vile vyuo vikuu. Nitoe mfano hai kwamba pale kwangu Musoma Mjini tunacho Chuo cha VETA, kimejengwa vizuri, lakini ukiangalia idadi ya namba za watoto ambayo wanachukuliwa pale ni wachache sana ukilinganisha na mahitaji, lakini wale watoto ambao wanasoma vyuo vikuu wapo wengi sana, lakini mwisho wa siku wanarudi mtaani hawana ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni vizuri Serikali ingejitahidi kuongeza vile vyuo kwa maana ya kuviongezea fani mbalimbali na wale watoto waweze kujifunza kwa njia ya vitendo. Leo ukienda pale mfano Musoma unakuta kuna gari moja, yaani wapo wanafunzi wanachukua kozi ya Umakenika, lakini gari lililopo pale ni moja tena bovu. Sasa wanafunzi karibu 200 waliopo pale, maana yake ni kwamba kuja kujifunza namna ya kufunga injini tafsiri yake ni kwamba vijana wengi wanatoka pale hawana ujuzi wa kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ndiyo maana tunasema hebu mjitahidi kuangalia namna bora zaidi ya kwanza kuvipanua hivyo vyuo na ikiwezekana viende kila Jimbo na vile vile mwendelee kuviongezea fani na facilities za kuwafanya waendelee kujifunza kwa njia ya vitendo. Kwangu mimi nadhani hilo linaweza likasaidia zaidi kwenye upande huo ili vijana wengi waendelee kupata ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, lipo suala ambalo tunahitaji tuendelee kuwasaidia wale vijana wetu wanaomaliza vyuo vikuu pamoja na vyuo vya kati hasa kwenye kada hii ya Ualimu. Leo Mheshimiwa Waziri akiamua hilo, nadhani linaweza likaleta impact ya haraka. Tanzania tuna bahati moja kwamba unapozungumza lugha ya Kiswahili, hii lugha ya Kiswahili sisi ndio waasisi wa hiyo lugha, lakini ukienda duniani katika nchi nyingine wako majirani zetu hapa wa Kenya wanatoa walimu wa kwenda kufundisha katika nchi nyingine lugha ya Kiswahili, lakini kumbe hiyo ni opportunity ambayo kwetu sisi kama Tanzania tungeweza kuitumia. Mfano watu wengi katika Mataifa mbalimbali wanachohitaji kujifunza ni kusoma, kuandika na kuongea lugha ya Kiswahili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, leo sisi hatulazimiki kutafuta wale Walimu ambao wamesomea Kiswahili peke yake, hao ndiyo wakafundishe lugha ya Kiswahili katika Mataifa mengine; kumbe watu tunaowahitaji ilimradi awe anajua Kiingereza, halafu anajua Kiswahili, maana yake ni kwamba anaweza akaenda na akafundisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, ungeniuliza tufanyeje? Tunaweza kufanya kitu kimoja kwamba katika zile ofisi zetu za mabalozi zote zilizopo katika nchi mbalimbali, tukaweka pale kitengo ambacho kinafundisha Kiswahili kwa muda mfupi. Kwa kufanya hivyo kumbe tunaweza tukawapeleka kule walimu wetu wengi na wakafanya kazi hiyo ya kuweza kuwafundisha Mataifa mengine. Kwa hali hiyo wakapata ajira na maisha yakaendelea kuliko hivi sasa ambavyo tunakaa nao humu pasipokuwa na ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, siku za nyuma wakati nakua, ilikuwa ukitembea huko duniani, ukikutana na asilimia kubwa ya watu ambao ni Watanzania walikuwa wa Taifa moja la Nigeria. Nigeria ilikuwa inasifika kwa kuwa na vyuo vingi karibu kushinda nchi nyingine yoyote ile, na hiyo ni kwa sababu wao walikuwa wanaonekana walikuwa na mfumo kama wa hapa kwetu na madhara yake makubwa ambayo walikuwa wanayapata walikuwa wanaonekana sio miongoni mwa nchi Taifa ambalo watu wake sio waaminifu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo inatokana na nini? Ni kwa sababu walikuwa wamesoma, lakini elimu waliyosoma ni elimu ya kusoma ambayo haiwasaidii katika ku-create ajira. Sasa mimi nina mashaka sana kwamba leo Watanzania wengi na kwa elimu tunayoipata ndiyo hiyo tu kwamba kila mmoja unakuta amemaliza Chuo Kikuu lakini haajiriki. Shida kubwa ambayo wanaipata hawa wasomi, hawezi kufanya hizi kazi za kawaida, lakini anafika mahali ajira zinazopatikana huwezi kuamini leo analipwa mpaka shilingi 300,000 mtu mwenye degree ya Chuo Kikuu.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)