Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, soko la nyimbo na muziki wa Tanzania linazidi kukua kwa kasi kwa sababu Watanzania wanapenda burudani, sanaa na kujifunza kupitia nyimbo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu tatizo la wasanii wa Tanzania kutofanikiwa kiuchumi; wasanii wananyonywa sana, wasanii wanapata faida kidogo huku hawa wasambazaji wakineemeka kupitia wasanii wetu. Lakini pia gharama za kurekodi kazi za wasanii wetu, muziki wa audio na video kurekodi gharama ziko juu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Serikali kusimamia hasa kwa wasanii wetu wapunguziwe gharama za kurekodi na kuzalisha kazi zao. Kuna wasanii wengi wanashindwa kuzalisha kazi zao kwa sababu kipato chao ni cha chini sana. Nini kifanyike? Kuanzisha studio ya Serikali ili kuendelea kuwainua wasanii wachanga wenye uwezo mzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wizi wa kazi za wasanii, Mheshimiwa Waziri Serikali ina uwezo kabisa kuzuia wizi wa kazi za wasanii hasa kuweka password katika nyimbo zao, CD, DVD ili hawa wasambazaji wakose mwanya wa kuiba kazi za wasanii ambao wanazalisha kazi zao katika mazingira magumu sana. Mheshimiwa Waziri, leo kuna baadhi ya studio ziko hapa nchini kurekodi video moja mpaka shilingi milioni saba, Je, Serikali haioni haja ya kudhibiti gharama hizi na wasanii wetu wakaweza kustahimili hizi gharama na nini kifanyike? Serikali idhibiti, soko la muziki hasa kwa hawa wamiliki wa studio mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la usajili wa haki miliki ya msanii, mzunguko wa kupata haki miliki ya msanii umekuwa ni mrefu sana, pia mzunguko wa kupata sticker ili kazi itambulike na usajili wa TRA. Hivyo basi, ninaomba Serikali kupunguza mlolongo wa usajili na pia kuweka ofisi za usajili kila Mkoa ili kupunguza mzunguko wa kupata hizo sticker za TRA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwako Mheshimiwa Waziri ni kuwashauri pia wasanii hawa wafanye kazi kwa ushirikiano. Nyimbo zifuate utamaduni wa Kitanzania, wasanii wasijiingize kufanya kazi za kisanii na siasa hii inashusha muziki wetu awe CCM, CHADEMA au ACT, wasanii wetu kujiingiza katika siasa kunashusha soko la Tanzania hususani muziki. Mfano wa nchi ambazo wasanii walishuka hasa kwa kuchanganya siasa na kazi za sanaa ni Zimbabwe na Congo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu rushwa katika mchezo wa mpira wa miguu na netball, Mheshimiwa Waziri chunguza kwa makini suala hili ili timu zetu zifanikiwe bila dalili za rushwa. Ngoma za jadi na ngoma za asili zisisahaulike kwa mustakabali kwa kutunza, kuendelea na kukuza utamaduni wetu na siyo kuendelea kukuza muziki wa kizazi kipya pekee.