Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia leo katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Kwanza kabla ya yote naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kutujaalia uhai.

NAIBU SPIKA: Ndiyo wewe au?

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya, leo hii nimesimama hapa kuchangia masuala ya elimu juu ya watu wangu ambao wamenileta hapa Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais, sana sana. Mama jana tumekusikia umezungumza kama Mama tena Mama yule ambaye ana viakiba vyake yupo tayari watoto wake wale hata ugali na mlenda kuliko kushinda na njaa. Kwa hiyo, tayari tumeona namna gani Mama anaguswa na Watanzania na wanyonge na tunakupongeza sana Mama, tunakupongeza sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie leo kwenye hii Elimu, Sayansi na Teknolojia juu ya masuala ya vipaji. Mimi ni muumini wa vipaji, kwa sababu nimepata kipaji changu, nilikuwa na kipaji changu lakini nimeendelezwa kupitia Shule ya Msingi. Nimefanya bands, nimefanya kwanya, nimeimba na nimefanya vitu vingi sana mashindano ya kwaya, bendi yakanijengea uwezo. Kwa hiyo ninaamini kabisa Wizara ya Elimu ikiangalia namna hii ya kuweza kukuza vipaji vya watu, leo hii tusingewaponda akina Diamond na wengine kwa sababu shamra shamra za shuleni za mashuleni zile za mashindano ya waimbani na vitu kama hivyo.

Kwa hiyo, naamini kabisa, Wizara ya Elimu ikiangalia namna hii ya kuweza kukuza vipaji vya watu, leo hii tusingewapata akina Diamond akina nani kwa sababu ya ile shamra shamra za shuleni zile za mashindano ya waimbaji ya nini na vitu kama hivyo. Kwa hiyo, naamini sio kipaji kimoja tu tunaweza tukakipata shuleni vipaji vingi tu tunaweza tukatengeneza watu wengi tu wacheza mpira, michezo, everywhere, kila sehemu tunaweza tukapata watu wa kuweza kuwakilisha hii nchi, lakini pia kuinua uchumi wa hii nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni muumini wa vipaji kwa sababu pia itaacha haya mambo ya kukaa vijiweni kuvuta bangi, kuvuta unga na panya road. Vipaji vitakuzwa kimaadili zaidi, tutaona kabisa umuhimu wa vile vipaji ambavyo tunavitengeneza kuanzia chini mpaka kwenda juu. Kwa hiyo, naiomba Wizara hii iangalie hilo kurudisha mambo ya muziki shuleni, mambo ya mpira michezo na vitu kama hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, cha pili naomba nichangie juu ya masuala ya lugha ya alama mashuleni. Juzi nimesema tunahitaji lugha ya alama mashuleni, ni muhimu sana. Tunafahamu kabisa lugha ni mojawapo ya sehemu ya mawasiliano, hatuwezi kuelewana kama hatutumii lugha ambayo tunaweza tukaelewana. Naomba tu niwaulize Wabunge leo hii Wabunge nyinyi humu ndani mnawawakilisha wananchi, watu wenye ulemavu huko chini katika Majimbo yenu, hivi ni wangapi humu ndani wanafahamu lugha ya alama ya kuwasiliana na viziwi? Wangapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni wachache sana, kama wapo basi ni mmoja, wawili au watatu, mimi mwenyewe sifahamu lugha ya alama na huwa najisikia vibaya sana. Kwa hiyo, ningeomba Wizara pia ilete semina hata ya wiki moja tufahamu tujifunze lugha ya alama, tujue numbers tujue vitu basic ambavyo vinaweza vikatusaidia kuwasiliana na hawa watu wasijione kama wanatengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo mpiga kura wako akija kwako anataka kuzungumza na wewe hawezi kuzungumza naye. Gharama za mkalimani ni kubwa sana, hawezi kumudu muda wote akawa anatembea na mkalimali ili akuelezee shida zake. Kwa hiyo, tunaamini kabisa watoto wetu mashuleni wakianza kujifunza lugha ya alama ina maana hata watu ambao wamezaliwa wana ulemavu wa kutokusikia, tayari itawasaidia wao. Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie hili ni muhimu mno mno, ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, cha mwisho, naomba nichangie juu ya masuala ya elimu jumuishi, tunafahamu tuna Walimu katika mashule ya elimu jumuishi. Tunafahamu kwamba hawa Walimu wengine ni wachache mno, lakini wengine pia wame-specialize kwenye area moja lakini sasa kwa sababu tu ni walimu wa elimu jumuishi, wanakwenda mashuleni wanafundisha kila mtoto ambaye ana matatizo ya ulemavu, hapana. Tunatakiwa tujue kabisa huyu mwalimu ame-specialize kwenye viziwi peke yake, huyu mwalimu ame- specialize kwenye ulemavu wa akili, huyu mwalimu ame- specialize kwenye area hii na hii na hii. Kwa hiyo, tujue namna gani hawa watu wanaweza wakatusaidia tuongeze Walimu ambao wamebobea katika sehemu mbalimbali ili tuweze kuwafundisha hawa watu na vile vile kuwatengenezea mazingira mazuri ya wao kuishi katika hii dunia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze mama katika area moja. Ameongeza vyuo vya watu wenye ulemavu sasa hivi vimeongezeka. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, amesema vyuo vilivyoongezeka kule Singida kesho kutwa tunakwenda kuzindua Tanga. Hii tayari ni hatua nzuri sana ambayo Serikali imefikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi vyuo tuvitumie hivi vyuo viende kuamsha/kuondoa umasikini wa watu wenye ulemavu tuwatengenezee elimu, lakini pia tuwape nyanja tofauti tofauti tuwatengenezee ubora na uwezo ambao wanaweza wakafanya. Hivi leo hii wanaonaje Serikali wakawafundisha hawa watu wenye ulemavu ambaye yeye labda hawezi kutembea, tukamfundisha kutengeneza bahasha tu hizi, halafu leo tender za hizi bahasha tukazichukua kwa watu wenye ulemavu, ndio tukawa tunawalipa wale watu wenye ulemavu, hatuoni kama tutakuwa tumewasaidia hawa watu wenye ulemavu? Kwa hiyo, naomba Serikali itafute namna gani ya kuondoa umaskini wa watu wenye ulemavu, watu wenye ulemavu ni maskini sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumze, hawa watu ni masikini sana, kwa sababu kama mtu tu ana miguu yake na mikono yake na maisha ni magumu, fikiria mtu ambaye hana miguu, hana mikono, hawezi kusikia, ni namna gani ambavyo anaishi au na wale pia familia ambayo inawalea wanashindwa kuwalea vizuri. Kwa hiyo, naomba Serikali inapokuwa inafikiria mambo yake ya kimaendeleo, mambo ya kielimu, iangalie sana kundi hili ni muhimu mno. Mmii ni sauti ya watu wenye ulemavu hapa Bungeni, nitazungumza kila siku na mtanichoka lakini naomba Serikali iangalie namna gani ya kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusema hayo machache naunga mkono hoja na nashukuru sana. (Makofi)