Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa nawashukuru Wizara ya Elimu chini ya Profesa Mkenda, kaka yangu, nawapongeza sana kwa juhudi kubwa mnazofanya kuhangaika katika kuhakikisha kwamba mnainua elimu ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukifuatilia michango ya Wabunge wote waliozungumza kuanzia asubuhi mpaka sasa hivi tunaelekea mchangiaji karibu wa kumi na kitu, utaona namna gani Wabunge wengi wamezungumzia changamoto ambayo haioneshi consistence katika mfumo wetu mzima wa elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania tunajua uwezo wa Mheshimiwa Prof. Mkenda na Naibu wako. Nchi inatambua ya kwamba yeye ni msomi, mzalendo aliyesomeshwa kwa kodi za Watanzania, ana uwezo mkubwa, ni zao la watoto wa kizalendo wa nchi hii. Tumaini la Watanzania ni kuona nchi inapata transformation kwa lengo la kusaidia sustainable development katika masuala mazima ya elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria Na. 25 ya mwaka 1978 imempa mamlaka Waziri wa Elimu kuunda chombo cha kisheria; Baraza la Ushauri katika masuala ya elimu katika nchi yetu. Ndugu zangu Watanzania na Wabunge wenzangu, nataka niwaambie with a very big disappointment; toka sheria hii imeundwa, hapa tunazungumza alikuja Waziri fulani akafuta hiki; akaja fulani, akafuta hiki; huyu anazungumza habari za mitaala; hivi leo tukiuliza, toka Sheria ya mwaka 1978, ni mwaka gani Serikali yetu tumetekeleza kuunda chombo chenye watalaam wazalendo wanaoona direction na vision ya nchi wakamshauri Waziri juu ya mwelekezo na mustakabali wa nchi katika elimu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, kaka yangu, Mheshimiwa Profesa Mkenda, tunakuomba ukawe shujaa wa kwanza Waziri katika Taifa letu utakayekwenda kutekeleza takwa hili la kisheria Na. 25 ya mwaka 1978. Nenda kaunde chombo cha kisheria, Baraza litakalokuwa linakushauri katika masuala mazima ya elimu. Hizi kelele unazozisikia kwa Wabunge, hautazisikia mpaka siku Yesu anarudi. Ni kweli watu wamekuwa wakijichukulia hatua na kufanya maamuzi bila ku-reflect demand na nini dunia inakihitaji hasa Taifa letu katika dunia tunayokwenda ya globalization. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni matumaini yangu Mheshimiwa Prof. Mkenda ninamshauri kama mdogo wako na kama Mbunge mwenzio, sheria imekupa mamlaka, tukimaliza ikiwezekana hata kesho teua watu watangaze tupate chombo cha kuanza kukushauri katika masuala mazima ya elimu. Hizi kelele za Wabunge hautazikisikia na utaona changamoto nyingi zinazozungumzwa kuhusu elimu yetu na mitaala, tutakwenda ku-harmonize na kulisaidia hili Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu wa pili; asilimia 25 ya sekondari katika Taifa letu zinatokana na private investmate kwa maana shule za private. Leo tunapozungumza, kaka yangu Mheshimiwa Innocent, Waziri wa TAMISEMI, nampongeza kwa huruma yake kubwa sana, juzi akaamua kuongeza nafasi ya watu kufanya application zilizotangazwa katika Serikali. Naomba Bunge lako linisikilize kwa makini; kama private sector inafanya asilimia 25 ya shule, Mheshimiwa Innocent juzi ametutangazia nafasi takribani 10,000. Kwa taarifa nilizonazo mpaka sasa hivi, waliyoomba ni zaidi ya waombaji kama 120,000 kwa nafasi 10,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu kwa Serikali, Profesa Mkenda kaka yangu mnisikilize. Tukitaka kusaidia changamoto ya upatatikanaji wa walimu kupata ajira na walimu wa masomo ya sayansi kuongezeka lazima private sector ipewe nguvu, na kwamba shule za private lazima zipewe nguvu. Leo tunapozungumza shule za private tumeziwekea mpaka cooperate taxi, jamani elimu hii ni huduma! Tukiweza kupunguza kodi kwenye shule za private mimi nakwambia tutasaidia Watanzania wengi kufungua shule, walimu wetu wanaokosa ajira wataajiriwa kwenye private. Tutasaidia kutatua changamoto kwenye Sekta ya Elimu na kaka yangu Mwigulu Madelu na ninaju upo hapa, ninajua hiyo kodi utakwenda kusaidia kuzifuta kwa lengo la kusaidia Private Sector Investment katika Sekta nzima ya elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu wa tatu. Serikali inachukua mikopo mingi, na ninampongeza sana Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan. Uwekezaji unaofanywa katika miundombinu ya elimu ni uwekezaji unaotia moyo sana. Rais wetu asivunjwe moyo aungwe mkono na apongezwe. Uwekezaji unaofanyika ni wa hali ya juu. Hata hivyo, ninaomba nikosoe na kushauri. Tuna programu za EP4R ambazo wastani tunakopa kama Dola milioni 500. Tuna programu EQUIP ambazo pia tuna Dola kama milioni 500.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hivi mtoto anayesoma private ni mtoto wa Kitanzania au siyo wa Kitanzania? Mtoto anayesoma shule ya Serikali anatafuta elimu ni wa Kitanzania au siyo wa Kitanzania? Tukitaka tusaidie Taifa letu kwenye suala la elimu, ninatoa ushauri, kwamba fedha za mikopo katika investment katika masuala ya walimu Serikali msione haya kuzisaidia shule za private katika investments, kwenye masuala ya vifaa, Maabara na walimu. Kwa sababu mikopo hii hata wale wa private wanalipa tusiwabague kwa lengo la kujenga hali ya kuwasaidia wananchi wetu kuweza kupata unafuu katika kupatikana kwa walimu katika maeneo hayo; huo ni ushauri wangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumza kaka yangu Erick Shigongo, nimekusikiliza kwa makini sana brother. Lakini kuna muda pia alizungumza Profesa asubuhi. Leo tunapozungumza ukienda katika vyuo vya Uganda, fanya research, nenda katika vyuo vya Makerere na Bukene, nenda kwenye vyuo vya Kenya kama vile Nairobi University, halafu njoo fanya comparison na vyuo vya Tanzania. Nenda kaangalie idadi ya Watanzania wanaosoma Kenya na Uganda na idadi ya waganda wanaosoma Tanzania, utakuta kuna huge gape. Sababu kubwa ya msingi bado tuna mediocracy mind set ya kung’ang’ania vitu ambavyo havilifungui taifa katika kufanya Taifa letu la Tanzania liweze ku-integrate na ku-absolve mambo mengine ya technological transfer yatakayosaidia nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano sisi tumeweka kigezo cha mtu kwenda Chuo Kikuu mpaka asome kidato cha sita. Hapo Kenya mtoto anamaliza kidato cha ana- qualify kwenda Chuo Kikuu akija Tanzania refraction. Haya mambo hayawezi kulisaidia taifa. Ushauri wangu ninaotoa Profesa Mkenda kaka yangu nenda kakae na timu yako. Na timu hiyo najua hata hili ninalolishauri, Baraza la kiufundi ambalo limeundwa kwa Sheria namba 25 ya mwaka 1978, ninajua kabisa ushauri ninaoutoka ukienda kuzungumza huko Serikalini mka-harmonize faida ya kuwa na integration ya watoto kutoka mataifa mengine kuja kusoma kwetu kwanza vyuo vikuu vitaongeza mapato ya kudaihili wanafunzi, pili tutaweza kurahisisha ku-harmonize technological transfer kutoka Mataifa ya wenzetu kuja kwetu lakini pia tutajiendelea kujenga mshikamano na undugu katika block zetu za kikanda na katika masuala mazima ya kisiasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu wa mwisho. Vyuo Vikuu, ninatoa ushauri tumeweka retirement age ya walimu wa vyuo vikuu...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili hiyo Mheshimiwa Kingu.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, naama.

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima yako.

NAIBU SPIKA: Sekunde mbili malizia.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kaka yangu. Ninatoa ushauri tumeweka retirement age kwa vyuo vikuu miaka 65, lakini nataka niwaambi kule vyuo vikuu mimi nilifundishwa na akina Profesa Kuzilwa walikuwa ni watu umri umeshakwenda. Wekeni taratibu watu wakishafikisha huo umri waanze kusaini mikataba, kule vyuo vikuu hawabebi zege, tunapoteza maarifa kwenye nchi, watu tunawaacha bado wana uwezo wanakwenda wanakaa nyumbani. Maprofesa… (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante, mengine andika kwa Waziri.