Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nitumie nafasi hii kwa fursa hii uliyonipa; na mimi naomba nichangie. Kwanza nisema naunga mkono hoja. La pili, niwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa ushauri waliotupa kwa upande wa Serikali na nataka tu niwahakikishie kwamba kwa Wabunge kusema wazi mawazo yao inatusaidia sisi upande wa Serikali kuweza kutambua na kuelewa kwamba kwenye planning zetu tunatakiwa kuchukua hatua zipi za muda mfupi na za muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli kwamba hatujitoshelezi kwenye mafuta ya kula. Lakini ni ukweli kwamba upandaji wa bei ya mafuta ya kula unasababishwa na mambo makubwa mawili. Yapo yaliyopo ndani ya uwezo wetu na yapo ambayo yapo nje ya uwezo wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama nchi tunatumia wastani wa tani 650,000 kwa mwaka ya mafuta ya kula. Uwezo wetu wa uzalishaji ni wastani usiozidi tani 250,000 – 300,000; asilimia 70 ya haya mafuta tunayozalisha yanatokana na mafuta ya alizeti. Linapotokea tatizo duniani kama lilitokea la COVID, Ukraine, upande mmoja ni balaa lakini upande mwingine ni fundisho ambalo sisi kama taifa na watanzania; linatufundisha kwa sababu hapa tulipo ni maamuzi tuliyoyafanya kama taifa miaka ya 90; tulipoamua kuacha ku-protect sekta yetu binafsi na ku-protect viwanda vyetu it was a policy na ilifanywa na watanzania wote; na sheria zingine zilipita ndani ya Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo baada ya matatizo ya COVID nchi inajadili kwa nini hatuna mafuta ya kula? Baada ya matatizo ya Ukraine nchi inajadili kwa nini hatuna mbolea? Si kwamba hakuna rasilimali, Tanzania ilikuwa na Tanzania Fertilizer Company tuliamua; kwa hiyo kama tumeamua kama nchi kutubu kurudi kwenye misingi let us take a responsibility as a country; isiwe kuinyooshea kidole Serikali, isiwe kuinyooshea kidole Serikali, Serikali ilitekeleza maamuzi yaliyopitishwa na Bunge hili hili na sheria zilipitishwa humu humu ndani. Tuliamua kwenda kwenye mfumo wa uholela; tukaua mambo yetu ya msingi kama nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Sita inachukua hatua gani? Moja, tunachukua two policy direction ambazo tunafanya Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Fedha. Cha kwanza, mwaka huu tumefanya pilot ya kugawa mbegu kwa mikoa mitatu; tumegawa kwa ruzuku. Nataka niseme na sisi tuwe wakweli kwa sababu siku ya mwisho we will all die, tutakwenda kuhukumiwa kwa Mungu. Dhana ya kufikiri Serikali haina jukumu la kulinda sekta binafsi kwa ku-protect viwanda vyake vya msingi ni dhana potofu. Kwa sababu sasa hivi all over the country wanainyooshea kidole Serikali and we forgot kuwa ni sisi ndio tuliamua kutokulinda viwanda vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Sita imeamua ku-protect na Serikali ya Awamu ya Tano ilianza; tume-protect sekta ya sukari kwa uweo wa Mwenyezi Mungu 2025 tutajitosheleza. Serikali sasa hivi kuhusu viwanda vidogo vidogo vya sukari tunafanya nini? Wizara kupitia Bodi yetu ya Sukari kwa kushirikiana na TEMDO tunatengeneza portal types small industries za ku-process metric tons 10 kwa siku ya miwa ambayo itatupatia tani 24 kwa mwezi ili tuweze kuwapa vyama vya Msingi vya Wakulima. Anayegharamia ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kazi hii inafanywa na TEMDO na tutatengeneza hivi viwanda vidogo tutawagawia wakulima ili AMCOS katika ngazi za chini waweze ku-process sukari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekit, tunafanya nini kwenye mafuta ya kula? Tumegawa mbegu tani 3,000 na mwaka huu kwa uwezi wa Mwenyezi Mungu mkipitisha bajeti ya Wizara ya Kilimo tutagawa certified seeds tani 5,000 kama ruzuku kwa wakulima. Lakini kugawa mbegu peke yake hakutoshelezi lazima viwanda viwe competitive; tumejadiliana na Wizara ya Fedha tunachukua hatua za kikodi ili kuvilinda viwanda vyetu vya ndani ili viweze kuzalisha mafuta ya alizeti na siku ya mwisho yaende sokoni. Hatutomaliza tatizo la kujitosheleza mafuta kwa mwaka mmoja; lakini kwa uwezo wa Mungu ndani ya miaka mitatu tutajitosheleza na tutakuwa na mafuta ya kutosha ya alizeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wameongelea sana sana suala la mafuta ya kula; hatua ya pili tunachukua kwenye palm oil. Ukienda kwa mama ntilie hakaangi vitumbua kwa kutumia mafuta ya alizeti, anatumia mafuta ya mchikichi; ukienda kwa mama ntilie anatumia mafuta ya mchikichi. Sisi kama Serikali hatua tunayochukua wakati tuna-develop kwa muda mfupi mafuta ya alizeti long term tunakwenda kwenye palm. Tumeanza kuwapa wawekezaji wakubwa maeneo makubwa kwa ajili ya kulima mchikichi. Kwa muda mrefu mchikichi na lazima tuelewe kuna kitu kinachoitwa economies of scale. Mchikichi hauwezi kuwa profitable kwa kulima heka moja halafu tukadhani kwamba yule Muha wa Kigoma anaye-crush mchikichi na kuzungusha kwenye pipa siku ya mwisho yale mafuta yataweza kuwa competitive sokoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachukua hatua gani? Tumepata wawekezaji wakubwa ambao tunawapa 10,000 hectares; moja tunampa Bakheresa hekta 10,000 down stream ya Rufiji kwa ajili ya kuweka michikichi, tuta-develop pembeni yake small scale farmers yeye ndiye atakayenunua na ku-crush ndipo pote duniani wanavyofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kule Kigoma tumegawa michikichi, Serikali inachukua hatua gani? Tutaweka viwanda vidogo katika eneo la Kigoma Manispaa ili miche tuliyogawa mwaka jana na mwaka juzi ambayo inakaribia ku-mature iweze kuweza kupata sehemu ya crushing. Nini nataka nimalizie, mimi nataka niseme jambo moja; suala la kilimo na kujitosheleza kwenye masuala ya msingi hasa mafuta ya kula, fertilizer, sukari ni suala la lazima. Tunawaomba Waheshimiwa Wabuge waiunge mkono Serikali kwenye hatua tunazoanza kuchukua kuanzia mwaka ujao wa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili suala la mbolea; ili viwanda viweze kupata rasilimali lazima mkulima azalishe; gharama za uzalishaji zikiwa kubwa mkulima hawezi kuzalisha na hata atakachozalisha kiwanda hakitaweza kununua. Kwa hiyo, ni lazima tukubali kama nchi tuanze kutoa ruzuku kwenye maeneo ya msingi na tuwaombe Waheshimiwa Wabunge Serikali inachukua hatua ya kupunguza gharama za riba, Serikali itachukua hatua za kikodi kuanzia mwaka ujao wa fedha kwa ajili ya kulinda industries ambazo ni muhimu; Serikali itachukua hatua ya kutoa ruzuku kwenye mbegu za mazao ya mafuta. Tutatoa ruzuku kwenye mbolea ije jua ije mvua tunawaomba mtuunge mkono kwenye hatua hizi; tuache kushauriwa kwamba Serikali haitakiwi ku-intervene kwenye maeneo ya msingi ni lazima tu-intervene this is the small economy, sekta yetu binafsi bado ni changa inahitaji Government intervention. Tutakapochukua Government intervention tunawaombeni mtuunge mkono kwenye masuala ya msingi ya kutoa subsidy. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.