Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuungana na viongozi wenzangu wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa majaliwa yake kwetu sote katika majanga mbalimbali na mafanikio katika nyanja za ustawi wa jamii, amani, uchumi, diplomasia na siasa za utashi mwema na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuungana na viongozi wenzangu wote kuwapa pole nyingi wale waliopoteza wapendwa wao katika kipindi chote hadi leo hii, tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu awapokee katika ufalme wake usio na mwisho mbinguni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha kwa namna ya pekee nachukua nafasi hii kuipongeza sana Serikali yetu ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano kwa jinsi inavyosimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020 hadi 2025, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kazi iendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nitoe mchango wangu katika Wizara hii muhimu kwa ustawi wa uchumi wa Taifa letu. Serikali yetu ifanye mapitio ya blueprint ili kutathimini wawekezaji wa ndani na nchi ya nje kwa ajili ya kuona inatoa hamasa kwani changamoto kubwa inayosababisha nchi yetu kutokuhimili upandaji wa bidhaa na mfumuko wa bei ni uchache mkubwa wa viwanda vya ndani vinavyotumia malighafi za ndani mfano wa wazi ni mafuta ya alizeti, sukari, kahawa na mengine, lakini husafirishwa nje ya nchi na baadaye kurudishwa ndani ya nchi baada ya kuchakatwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu ihamasishe uwepo wa wawekezaji wakubwa wa viwanda vya dawa, pembejeo za kilimo na uchimbaji wa mafuta na gesi kwani matukio ya janga la corona na vita vya Urusi na Ukraine na mengine mengi iwe ishara kwa Taifa letu kujifunza athari za majanga katika uchumi wa Taifa letu na kuepuka uagizaji mkubwa wa bidhaa zinazoweza kuzalishwa ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha nadhani ni wakati muhimu sana Wizara yetu ione kupata tathimini ya viwanda vidogo 100 vilivyoanzishwa kwa kila Halmashauri kwani bado kwenye maeneo ya vijijini kuna malighafi nyingi za kutengeneza na kuchakata na kufungasha bidhaa za matumizi za majumbani kama subuni ili kupunguza mahitaji madogo madogo na kuchochea ajira mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja kwa asilimia mia.