Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapongeza jitihada za kuendeleza michezo ingawa haijafika mahali inapotakiwa kwani tunaporomoka Kitaifa na Kimataifa kwa sababu vijana wetu hawana maandalizi ya awali na endelevu kwa fani maalum.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya maendeleo ya michezo haikidhi mahitaji katika kuimarisha miundombinu na mazingira kwa kuleta ufanisi katika michezo. Kwa ujumla bajeti ya Wizara haitoshi, inahitajika kuangaliwa upya mwaka ujao wa fedha 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuandaa watalaam wa kuwaandaa vijana wetu shuleni kuanzia ngazi ya shule za msingi na sekondari. Chuo cha Maendeleo ya Michezo - Malya pekee hakitoshi kuandaa watalaam wa kutosha kuwasambaza kwenye shule hapa nchini, ni vema Serikali kuona umuhimu wa kupandisha daraja vituo vya michezo kuwa vyuo vya maendeleo ya michezo kuongeza hao watalaam ili kuinua michezo na Taifa kufahamika duniani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kufahamishwa kwa nini Chuo cha Maendeleo ya Michezo - Malya na vituo vya michezo Arusha na Songea hawakuwekewa makadirio ya mishahara 2016/2017?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uhuru wa vyombo vya habari vilivyokithiri hapa nchini kwa upande wa magazeti ambayo baadhi yana poromosha maadili ya vijana wetu, Serikali ni bora kusitisha usajili wa magazeti na kuyafuta yanapobainika kwenda kinyume na maadili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.