Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana na mimi kunipa fursa hii ya kuweza kusimama kwenye Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya kuimarisha biashara zetu ndani ya nchi, pia niwapongeze sana Naibu Makatibu Wakuu pamoja na Katibu Mkuu kwa uandaaji mzuri wa taarifa hii na kuwasilisha hapa leo Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki nizungumze sana lakini zaidi nataka nijikite kwenye zao kuu la mwani. Zao kuu la mwani ni zao la kibiashara ambalo sisi kama Taifa tunategemea soko kubwa sana kupitia wenzetu wa Zanzibar pia kupeleka nje ya nchi zao hili la mwani. Pia kuna asilimia kadhaa ambayo tayari inabakia hapa kama malighafi kwa ajili ya utengenezaji na uchakataji wa sabuni, viyoyozi, cosmetic product pamoja na masuala ya kula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la mwani ni kama mazao mengine kwa mfano karafuu zao la korosho, ufuta na mazao mengine tofauti tofauti lakini ni jambo la kushangaza kuona kwamba zao la mwani halijapewa kipaumbele Zaidi. Naweza nikasema kwamba zao hili linaonekana kama labda wakulima wa mwani ni watu ambao wako kwenye hali duni ya kipato chao ambacho wanachokiendesha kwa ajili ya kulivuna zao hili la mwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kwamba zao hili la mwani kupitia Wizara hii bado halijapewa kipaumbele zaidi mbali na jitihada kubwa ambazo zinazofanywa kupitia na wenzetu wa TANTRADE lakini pia kuna wenzetu wa TIRDO wamefanya intervention kubwa na hivi juzi tu mwezi wa tatu tulienda pale TIRDO Dar es salaam, tukaona kuna sample zaidi ya 99 wamezichukuwa kwa ajili kufanyia utafiti, lengo hasa na madhumuni ni kuona kwamba hili zao la mwani linakuwa na soko lakini pia lina toa product ambazo tayari zitatumika ndani ya nchi lakini pia zitatumika ndani ya nchi lakini pia zitatumika nje ya nchi, hivyo nawapongeza sana TIRDO.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali na hilo pia niwapongeze sana TIRDO na kuwapa salamu za akina Mama kule Kisiwani Pemba kwa kuwajengea majokofu kwa kiingereza tunaita seaweed dryer majokofu ambayo especial kwa ajili ya ukaushiaji wa ule mwani ili mwani ukishakaushwa ukitoka pale utatoka mzuri lakini hautakuwa na vimelea vyovyote ambavyo vinaweza vikaathiri kwa hiyo niwapongeze sana ndugu zangu wa TIRDO kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niwapongeze sana ndugu zangu wa TANTRADE kwa kuona kwamba kuna umuhimu mkubwa sana ndugu zetu hawa akina Mama ambao ndiyo asilimia 90 wanajishuhulisha na zao hili la mwani wanawapatia fedha pia wanawapa elimu. Wamefanya kazi kubwa ingawa bajeti yao tunafahamu ni ndogo lakini wanafanya kazi kubwa mno kwa ajili ya kuwasaidia hawa akina Mama, ndiyo maana leo hii ukipita kwenye maonyesho ya Biashara kama utaenda Zanzibar ama utakuja Tanzania Bara bidhaa ambazo zinaonekana kushamiri kwa wingi kwenye maonyesho ya biashara ni bidhaa ambazo zinatokana na hizi za mwani, hivyo ninawapongeza sana ndugu zangu wa TIRDO. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado tunahitaji nguvu kazi kubwa kwa ajili ya kulinusuru zao hili la mwani. Zao hili la mwani tukilisafirisha nje tunaingiza pesa nyingi za kigeni na tukizibakisha hapa tunaingiza fedha nyingi za Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia zao hili la mwani limetengeneza fursa za ajira hususani kwa kinamama ambao wako kando kando ya bahari, tunayo mikoa i zaidi ya minne kwa Tanzania Bara, lakini kwa Zanzibar kuna mikoa mingi sana ambayo tayari inashamiri kwenye zao hili la mwani, lakini jitihada za Serikali bado zinaonekana ndogo kwa ajili ya kutafuta masoko. Zao hili la mwani miaka ya nyuma lilikuwa na thamani kubwa, katika matajiri ambao tayari utakaowazungumza kando kando ya bahari, basi ni wakulima wa mwani, lakini sasa hivi zao letu hili la mwani limedharaulika, limedharaulika kupita maelezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba sana Wizara iliangalie tena zao hili la mwani. Zao hili la mwani linanusuru asilimia 90 akinamama ambao tayari wako kando kando za bahari, hawana shughuli nyingine yoyote ya kufanya isipokuwa kulima zao hili la mwani. Kama Serikali kuna umuhimu mkubwa sana tukakaa kwa pamoja kuangalia masoko ya nje na ya ndani ili mradi zao hili la mwani kuliongezea thamani ili akinamama wale wasikate tamaa na kuweza kumudu familia zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina ushauri kupitia zao hili la mwani ili sasa lizidi kupata soko, pia tuweze kupata fedha za kigeni. Jambo la kwanza; tuna makampuni machache ambayo tayari yananunua mwani. Kwa hiyo, Serikali lazima tuangalie makampuni haya kunaonekana kuna urasimu wa hali ya juu, wanajipangia bei wanayoitaka wao wenyewe, hali ya kuwa kwamba ukiangalia kwenye soko la kidunia mwani una value kubwa lakini pia una fedha ndefu, lakini makampuni ambayo tayari yamepata accreditation kwa ajili ya kununua huu mwani ni makampuni machache. Hivyo naiomba sana Serikali iangalie namna ya kuruhusu makampuni mengine yote duniani yaje kununua mwani Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakinunua mwani hapa nchini kwetu naamini kwa asilimia 100 mwani utapanda bei na wananchi wetu ambao tayari wako hali duni za kiuchumi, basi wanaweza wakauza huu mwani kwa bei iliyokuwa ni nzuri. Kwa sasa hivi makampuni mawili kununua mwani, ni sawasawa na kufanya biashara ya monopoly, si sahihi kwa nchi yetu ya Tanzania wakati value of money ni kubwa, lakini mwani unanunuliwa kwa wingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, niwaombe sana ndugu zetu wa TANTRADE tunao ma-expert, tunao wataalam, tuwatumie hawa kwa ajili ya kushuka chini kwa wakulima wetu kwenda kuwapa elimu namna gani ya kuchakata huu mwani ilimradi kwamba tupate bidhaa bidhaa ambazo tayari tutaziuza kwa thamani iliyokuwa nzuri ili mradi kwamba sasa wakulima wetu waweze kuuza huu mwani, wapate fedha na kuendesha familia zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu; elimu ya ujasiriamali ya hali ya juu nayo pia itolewe, bado wakulima wetu elimu yao ni ndogo sana kwa ajili ya uchakataji wa huu wa mwani ili mradi kutoa bidhaa ambayo tayari itakayouzika. Kwa hiyo naomba sana watumie taaluma ya hali ya juu, watafute watu wa marketing, kisha warudi kwa wakulima wetu, bidhaa ambazo tayari wanazizalisha kule mitaani, basi wazifanyie marketing, wazi brand. Pia zipate national identity, zijulikane hizi bidhaa zinatoka nchini Tanzania. Tukifanya hivyo zao letu hili la mwani litapata value kama mazao mengine kama vile yalivyo mazao ya korosho, karafuu na mazao mengine yaliyokuwepo duniani.

Mhehimiwa Mwenyekiti, jambo la nne, kuna mfumo wa stakabadhi ghalani ambao umejikita zaidi kwa mazao haya ya biashara. Zao la mwani pia ni zao la biashara, hivyo naomba sana mfumo wa stakabadhi ghalani nao utumike kwa ajili ya kununua mwani, lakini mwani ukishanunuliwa, lazima uwekwe stoo ili mradi wanunuaji lazima waje kununua mwani kwenye stakabadhi ghalani. Tukifanya hivyo, naamini kwa asilimia 100 zao hili la mwani litakuwa kubwa, lakini pia wakulima wetu watashukuru sana kupitia haya mambo ambayo tumeyafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache, nakushukuru sana na naunga mkono.(Makofi)