Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, kuhamisha Gereza la Mgagao Kilolo na kuifanya sehemu ya makumbusho; kama Mjumbe wa Kamati napongeza jitihada za vyombo katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao. Lakini pia viongozi wa Wizara hasa kwa ushirikiano na Kamati na wepesi wenu katika kupokea ushauri na ambavyo mko accessible.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa ushauri ambao nimekuwa nikiutoa na kuuleta karibu kila mwaka, nawaomba sana mfikirie sana kuhusu kuhamisha gereza hili ambalo kwa mujibu wa historia, viongozi waliokuwa wapigania uhuru wa nchi za Kusini mwa Afrika walipata kuishi hapo kiasi kwamba watu wengi wakiwemo Mabalozi wa Afrika Kusini hapa nchini wametamani sana kupafanya eneo la kukumbuka historia yao, jambo hili tukiunganisha na jitihada za Mheshimiwa Rais kupitia Royal Tour, litasaidia kuvutia watalii.

Mheshimiwa Spika, nafahamu kwamba jambo hili linagusa Wizara zaidi ya moja ikiwemo Maliasili na Utalii na pia Wizara ya Ardhi, hivyo nashauri Wizara ya Mambo ya Ndani iwe kiongozi katika hili ili lifikie mwisho.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.