Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, nitoe pongezi kwa Mheshimiwa Waziri Engineer Masauni na wasaidizi wake wote.

Mheshimiwa Spika, kuna baadhi ya magereza nchini ni ya zamani sana na ni hatari kwa maisha watu. Mfano ni Gereza la Sumbawanga Mjini.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Nyasa ni kubwa na ina milima mingi. Urefu wa mwambao ni kilometa 157, umbali ukanda wa juu hadi Mitomoni kilometa140. Pia sisi tuko mpakani na Msumbiji na Malawi.

Kuhusu magari, yaliyopo ni chakavu. Mimi mwenyewe niliona umuhimu nikawachangia pikipiki nne.

Mheshimiwa Spika, tafadhali naomba msaada wa gari na nawasilisha.