Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Amiri Mkuu Jeshi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na pili niipongeze Wizara na hasa Mheshimiwa Masauni na Mheshimiwa Sagini.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kuhusu Gereza la Keko; hili gereza limekuwa la zamani na miundombinu yake hairidhishi kwani mahabusu ni wengi kuliko linavyoweza kubeba mahabusu hitajika kwa ukubwa wake. Naomba kuishauri Serikali kwamba ifanye maboresho ya gereza na ikiwezekana liongezwe kulingana na mahabusu wanaoingizwa pale ili kuweka hali ya afya yao vizuri, lakini pia Maafisa Magereza wanaoishi pale nyumba zao haziridhishi kwani ni chakavu pia magari yao ni ya muda mrefu. Niiombe Serikali iliangalie suala hili kwa makini.