Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Awali ya yote naunga mkono hoja iliyowasilishwa.

Mheshimiwa Spika, pili nataka tu kukumbusha Wizara kwa maana Waziri tulishafanya mawasiliano kadhaa kadhaa kuhusu Wilaya yetu ya Malinyi kuna shida ya usafiri kwa maana ya Polisi wanahangaika namna ya kufanya kazi. Kwa hiyo, nilishafanya mawasiliano rasmi na Ofisi ya Waziri ninaamini wanalifanyia kazi ninawakumbushia tu. Mtu yoyote akisikia Malinyi afahamu maana yake ni Wilaya ambayo ina ukubwa zaidi ya mara nne ya ukubwa wa Dar es Salaam yote. Kule kuna migogoro mikubwa sana ya wakulima na wafugaji hali ambayo inaleta ugumu Polisi kufanya mobility kufika kila angle. Malinyi inakaribia square meter 10,000 kwa hiyo unaweza ukaona zaidi ya mara tano mara sita ya Dar es Salaam na maeneo mengine. Kwa hiyo, uhitaji ni mkubwa sana kwa ajili ya sisi kusaidika, kwa hiyo niombe tu Mheshimiwa Waziri atoe kipaumbele mgao wa magari ambao utakuja lakini hata kama yapo mahali ya akiba yaliyotumika sisi tutayapokea uhitaji ni mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili suala la Jeshi la Magereza. Tumeangalia hapa katika taarifa yao kuna masuala mengi tu kuna sehemu bajeti zimewekwa za ujenzi wa Magereza, lakini naamini bado haitoshelezi. Mimi ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya masuala ya UKIMWI, tumefanya ziara Magereza mengi msongomano ni mkubwa sana, sana. Mahabusu ni wengi kuliko wafungwa wenyewe, sasa hili jambo limekuwa maarufu tangu mimi nikiwa mdogo tunasikia msongamano, msongamano lakini sijaona jitihada kubwa ile ya moja kwa moja ya kumaliza changamoto hii. Nimeona kwenye taarifa wameandika kuna masuala mengine vifungo vya nje na kadhalika, lakini bado uhitaji wa Magereza ni mkubwa. Hata tuweke kwa bajeti kwa namna gani Jeshi la Magereza halitokaa kamwe liweze kujenge Magereza ya kutosha. Wizara ya Mambo ya Ndani peke yake hata tuiache yenyewe haitoweza kumaliza changamoto hii. Kwa hiyo nilikuwa natoa ushauri kwa Serikali suala la ujenzi wa Magereza iwe kampeni ya Kitaifa kuisadia Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, mtakumbuka tulisadia kwa pamoja kampeni ya ununuzi au ujenzi wa madarasa. Mheshimishiwa Rais ametoa fedha tumejenga madarasa kila mahala lakini hata kampeni ya madawati mtakumbuka miaka miwili, mitatu iliyopita ilikuwa ni ajenda ya Kitaifa siyo suala la TAMISEMI, wala siyo suala la Wizara ya Elimu kila mdau, kila Taasisi iilipambana kuhakikisha tunafakisha jambo hili na tulifanya sehemu kubwa, ninaomba nguvu ileile iletwe Wizara ya Mambo ya Ndani tuisaidie Jeshi la Magereza kuweza kupata Magereza mengi.

Mheshimiwa Spika, Malinyi tuna maeneo makubwa kama kuna uhitaji tuko radhi kutoa maeneo kule Magereza kule ijengwe. Lakini naomba tu wale ambao hawajawahi kutembelea Magereza wajue kule hali ni mbaya sana. Kwa sababu Magereza wateja hawapelekwi kwa hiyari kama shuleni, au hawaendi kwa hiyari kama hospitali ndiyo maana Taifa linaweza lisione ukubwa wa changamoto ya msongamano. Lakini suala la shule kila mtu anaguswa kwa sababu anapeleka watoto, Hospitali, Zahanati kila mtu anapeleka kule wagonjwa ndiyo maana tunaona kila siku, lakini Magereza ni tofauti. Kwa hiyo niombe tu Serikali suala la ujenzi wa Magereza iwe kampeni ya Kitaifa. Ahsante. (Makofi)