Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa mchango wangu kwa waandishi wa habari kwamba wamekuwa na mazingira magumu ya kufanyia kazi na Serikali haijaweka mazingira mazuri ya kiajira na kimaslahi kwani hali hii inadidimiza tasnia hii ya habari, kuna wakati waandishi hulazimika kufanya kazi na kutoa habari ile ambayo haina maslahi kwake na kwa umma, ila ni kwa kuwa tu hana ajira inayoeleweka na mkataba wa kudumu. Hivyo ni kuidhalilisha tasnia hii, kwani mara nyingi wamekutana na risk mbalimbali za kimaisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishauri Serikali isaidie kuwapa mwelekeo mzuri waandishi hawa ambao pia wanasaidia Taifa katika kuelimisha jamii.
Pili, TBC ingeangalia pia kuweza kuongeza channel na pia kutokana na hayo, ni vyema ikaongezewa fedha ili ifike katika Wilaya 82 kama ilivyo katika bajeti yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, Taasisi ya Sanaa ya Bagamoyo inatoa stashahada, lakini Serikali haijaweka mitaala katika shule za chini ili somo la sanaa liweze kupanda kielimu. Masikitiko yangu ni kuwa Serikali imeanzisha taasisi hii bila kuwa na base au msingi toka chini. Kwa hiyo, naitaka Serikali ije na majibu ya kina kuhusu suala hili.