Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

Hon. Jumanne Kibera Kishimba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kahama Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza niwapongeze Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, rafiki yangu daktari, ingawaje sasa hivi haonekani toka amepata uwaziri. Nawapongeza sana pamoja na wafanyakazi wa Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, dhahabu ni kama ilivyo petrol na diesel, sisi kwa sasa hivi tunavyo-treat dhahabu tunai-treat kama bidhaa ya viwandani. Utajiri wa Waarabu ni pale mafuta yanapopanda, anayenufaika ni nchi ile kwenye ile difference ya kile kilichopanda. Bei ya dhahabu kabla vita ya Ukraine haijaanza ilikuwa ounce moja dola 1,800, lakini siku bomu limedondoka moja bei iliruka mpaka 2100, ongezeko la dola 300 ambayo sawasawa na dola 10 kwa gramu.

Mheshimiwa Spika, hoja yangu hapa ambayo najaribu kuijenga, je, hiki kilichoongezeka ni mali ya nani? Kwa sababu yule mwenye mgodi alikuwa anachimba na anapata faida na hiki kilichopanda hakikupanda kwa gharama ya uzalishaji, kilipanda kwa hofu iliyoingia duniani. Kwa wenzetu fedha hizo ni mali ya Serikali asilimia 100. Nasema hivyo kwa sababu mwenye mgodi hawezi kulalamika kwa sababu yeye gharama ya dhahabu haitokani na bei unayouza, inatokana na wewe unavyoendelea. Kwa hiyo bomu lilipodondoka bei ya dhahabu ilipanda muda uleule na tofauti iliyopo hapo kwa uzalishaji wa dhahabu kwa Tanzania ambao ni karibu tani 45 kwa mwaka, ni sawasawa na dola milioni 40 kwa mwezi. Pesa hizo kwa rate ya leo ni sawasawa na bilioni 200 kwa mwezi. Ni tofauti ya bei iliyotokea baada ya bomu kudondoka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wenzetu Waarabu ndicho kinachowapa utajiri, hatajiriki BP, anatajirika yeye mwenye mali. Ni hesabu rahisi haiitaji elimu kubwa sana; ukiweka mpunga kwenye mashine ya mtu au ukaweka alizeti ukasuburi kuja kukamua, inapopanda bei ya alizeti anayenufaika au mpunga anayenufaika ni yule mwenye mpunga si mwenye mashine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tuwaombe wenzetu wa wizarani kwasababu elimu hii ya madini najua wakati mwingine tukiongea elimu kuna kuwa na mvutano. Elimu hii ya madini ni mpya kwenye Idara zetu na kwenye shule zetu, kwa hiyo tuwaombe watalaam kama wanaweza kushauriana na hao wenye mgodi na hawawezi kukataa na hata tukiziacha hizi pesa, si kwamba mwenye mgodi atanufaika zitatengenezewa matumizi mengine ambayo yatazamia humo ndani. Kwa kawaida hizi pesa ni mali ya Serikali, zinaweza zikatusaidia mno. Zinatosha kabisa kutibu watu wetu bure kwa mwaka na kuwapa chakula cha mchana hata watoto wetu wa shule. Tuwaombe sana wenzetu wa madini wafikirie sana suala hilo kama wanaweza kulipeleka linaweza likatusaidia hasa sisi tunaotoka maeneo ya madini.

Mheshimiwa Spika, nilitaka kuchangia hayo tu. Baada ya mchango huo, nashukuru sana. (Makofi)