Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

Hon. Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia katika Wizara ya Madini.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na nzuri ambazo anazifanya katika nchi yetu. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri Doto Biteko na timu nzima ya Wizara ya Madini kwa namna ambavyo tunaona wanavyochapa kazi na kuhakikisha kwamba rasilimali hii muhimu katika Taifa inaendelea kuwa ni chanzo cha mapato kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza ndugu Fabian Mshai RMO wa Mererani pamoja na timu nzima ya watumishi Mererani. Pia niishukuru na kuipongeza Serikali kwa kuamua sasa soko la Tanzanite litoke Arusha na kuletwa Mererani wilaya ya Simanjiro katika mkoa wa Manyara. Vilevile nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuja kulizindua soko la madini katika mji wa Mererani Simanjiro ndani ya mkoa wa Manyara.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi za kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuja kufungua soko hilo niendelee kumshukuru na kumpongeza kwa uzalendo wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika kutengeneza filamu ya Royal Tour ambayo moja ya maeneo ambayo yalitumika ni pamoja na mji wa Mererani katika machimbo yanayochimbwa Tanzanite tunamshukuru kwa uzalendo wake kwa kutangaza tanzanite ulimwenguni kote kwa sababu wapo watu waliokuwa wakipotosha tanzanite haitoki Tanzania, tanzanite haitoki Manyara.

Mheshimiwa Spika, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kulinda urithi wetu, wa nchi yetu ya Tanzania kwa kuitangazia dunia tanzanite ni ya Tanzania tanzanite inatoka Manyara, tanzanite inatoka Mererani.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo, iliamuliwa kwamba sasa soko lijengwe Mererani tunaomba mchakato wa ujenzi wa soko ufanyike kwa haraka kwa sababu tayari maamuzi ya viongozi wetu wakuu wa nchi yalishafanyika na walishatoa maagizo. Ujenzi huo utasaidia sana kurahisisha ajira kwa vijana wengi. Sasa, tunaomba Wizara ya Fedha sasa taratibu zote zimeshakamilika michakato yote imeshakamilika iliamuliwa kutolewa bilioni 5 lakini kwa kuanzia ilitakiwa itolewe fedha kiasi cha bilioni 20.

Mheshimiwa Spika, unapotetea maslahi ya mkoa unaotoka, unapotetea maslahi ya vijana kuna wakati mwingine kidogo ... naomba niendelee...

(Hapa Mheshimiwa Asia A. Halamga aliacha kuongea kwa muda mfupi)

SPIKA: Haya Mheshimiwa Halamga nakutunzia dakika zako pumua kidogo kaa kidogo achangie Mbunge mwingine utarejea kumalizia hoja yako.

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, naomba niendelee

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, naomba niendelee niko vizuri kijana wako.

SPIKA: Haya ahsante sana.

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante Wizara ya Fedha inaendelea kutucheleweshea kutoa fedha hiyo, ambapo inatakiwa itoke bilioni moja kwa ajili ya kuanza ujenzi. Tunaomba Wizara ya Fedha wasikwamishe jitihada za Mheshimiwa Rais na hiyo fedha itoke ili ujenzi uanze. Lakini pia tunaipongeza Wizara kwa sababu baada ya soko hilo kukamilika kule ndani kuna package za mafunzo mbalimbali juu ya uchakataji wa madini pamoja na upandishaji thamani vito kwa ajili ya vijana. Hivyo itasaidia kuendelea kutoa fursa za ajira kwa vijana wetu wengi.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Manyara ni mkoa uliobarikiwa kwa madini, yako madini ya aina mbalimbali. Tuiombe Wizara sasa kuendelea kufanya utafiti kwa sababu tunayo madini ya grafit yako wilaya ya Hanang, tunayo madini ya green garnet yapo Mererani, tunayo Mabel kwa ajili ya tiles yapo Simanjiro, tunayo gold inayopatikana Basutu, tunayo madini Babati vijijini, tunayo madini wilaya ya Mbulu. Mkoa mzima wa Manyara umejawa na rasilimali hii muhimu katika nchi yetu, tuombe Wizara itoe hela ya tafiti.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kwa kumalizia tunaiomba Serikali, kile kinachotokana na madini tuombe Serikali irudishe fedha kwenye jamii kwa maana ya huduma za afya, barabara pamoja na maji. Lakini pia Mji wa Tanzanite City…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ASIA A. HALAMGA: ahsante naunga mkono hoja kwa asilimia zote. (Makofi)