Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nadhani nina dakika kumi, kwa hiyo, nitakuwa na kengele mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni hivi, kwanza kabisa huyu Mbunge ambaye amemaliza kusema nitumie dakika yangu moja kuwasaidia wanaopanga mambo ya madini. Tanzanite tulijaribu kuweka Centre kubwa iwe Arusha na tukaweka mitambo ya kuchonga na kuongeza thamani. Sasa ukisema madini yale yasiende Arusha, basi ile mitambo ya gemology yote inakuwa redundant. Ni hilo tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mchango wangu wa kwanza kabisa kwenye hii Wizara, naunga mkono tupitishe bajeti, wafanye kazi. Kama kawaida yangu, mimi natoa mawazo mapana zaidi. La kwanza ni kwamba, naomba hii Wizara ifanye kazi na Benki Kuu na tuweze kuanza kuwa na gold reserves. Maana ya kuwa na gold reserves, yaani kutunza dhahabu kwenye Benki Kuu yetu, kwa sababu kubwa tatu. Kwanza kunaimarisha sarafu yetu ya shilingi, halafu inasaidia mfumuko wa bei, na tatu ndiyo reserve ambayo inaaminika haina risk ya aina yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuthibitisha hiyo point, angalieni wakubwa duniani reserves walizonazo. Wa kwanza ni Mmarekani dunia nzima ana gold reserve tani 8,133; wa pili ni Mjerumani, ana reserve ya gold tani 3,359; wa tatu ni Italy; wa nne ni France; wa tano ni Urusi, ana tani 2,302; na wa sita ni China, ana tani 1,948. Sasa hawa wakubwa ambao wana uchumi mkubwa, wanalinda uchumi wa nchi zao kwa kuwa na gold reserves, kwa nini sisi Tanzania tusifanye hivyo? Hilio ndilo pendekezo na ombi langu la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa linganisha na nchi zinazotuzunguka. Msumbiji ambao tunawazidi uchumi, wana gold reserve ya tani 3.94; Burundi ambao tunawazidi, reserve yao ni 0.03 tons; Kenya ambao wanatuzidi uchumi, wao wana reserve ya 0.02 tons. Kwa hiyo, ni kwamba kwa kuwa tunakuwa na refinery nzuri sana kule Geita ambayo tutaweza kufanya purification ya gold kufikia 99.99. Kwa hiyo, ni muda muafaka sasa sisi kuwa na gold reserves zetu. Pendekezo langu la kwanza hilo.

Mheshimiwa Spika, la pili, tumeambiwa kwamba, baada ya Covid kuja sasa ndiyo tunapata takwimu sahihi. Wanasema uchumi ulishuka ukafika 4.8, sasa tuko 4.9. Ni lazima turudi seven twende eight na ikiwezekana ten percent.

Ndugu zangu Watanzania, uchumi usipokua kwa kadiri ya kiwango cha 8%, 10%, 10% na kuendelea hatuwezi kufuta umasikini nchini. Kwa hiyo, kitu kitakachotusaidia hapa ni kwenye sekta za uzalishaji muhimu; kilimo, uvuvi na ufugaji. Kingine ambacho kitatusaidia, ni lazima twende kwenye uchumi wa gesi, tupende tusipende, twende huko. Cha tatu, ni kwenye madini sasa. Haya Mheshimiwa Waziri ameyasema, sawa, tuendelee; ni dhahabu, vito na gemstones, lakini kwa miaka 20 inayokuja hapa duniani, madini yanayotakiwa hatujaanza kuyachimba sisi. Kwa hiyo, geological survey aliyokuwa anaiongea, tuipatie hii kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wabunge, geological survey ya Dodoma kabla ya mwaka 1961 wa Uhuru, ndiyo ilikuwa geological survey kubwa ambayo nchi nyingine walikuwa wanaleta watu wao kufanya mafunzo hapa. Tuiwezeshe hiyo. Geological survey kwangu mimi ni muhimu kuliko hii Tume ya Madini, ni muhimu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa madini ambayo tunapaswa kuyashughulikia kwa ajili ya kutoka 4.9% twende 8% economic growth rate, twende 10%, twende kwenye helium. Sikumsikia Waziri anaongelea helium gas. Hii gesi haiko Nishati. Kwa taratibu za nchi yetu, helium inasimamiwa na Wizara ya Madini, kama sijakosea. Sasa hivi hii helium ambayo iko nyingi huko Rukwa, global demand, duniani zinatumika six billion cubic feet. Duniani wanahitaji six billion cubic feet of helium per annum na growth yake itafika mpaka 10%. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka kesho soko la helium litakuwa na thamani ya 16 billion US Dollars na mtumiaji mkubwa ni NASA, anatumia 100,000,000 cubic feet per annum.

Kwa hiyo, naomba twende kwenye helium tuiendeleze. Hata hivyo, na yenyewe itakuwa kama ile ya LNG amabyo inabidi tuipeleke kwenye kimiminika (liquid). Tui- liquefy ile kule Lindi mpaka kwenye temperature ya -161.5, hiyo ni LNG, lakini helium ya Rukwa ni lazima tui-liquefy iende -2.69 degrees celsius. Haya siyo mambo ya mzaha. Minus! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa madini yanayohitajika duniani yatatumika kwenye magari, kwenye aerospace, military, clean energy na fourth industrial revolution. Wachina wamesema kufika mwaka 2025 wanataka kuachana na magari ya mafuta, wanahitaji madini. Madini ambayo yatahitajika kwa miaka 20 inayokuja, naomba niyataje; ni cobalt, chromium… (Makofi)

Aah, msipige makofi yasikike vizuri. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ni cobalt, chromium, lithium, palladium, nickel, zink, manganese, gallium, germanium, indium. Halafu na hii platinum group elements pamoja na rea earth elements. Kwa hiyo, naomba tukawekeze huko. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, madini mengine ambayo tunapaswa kuwekeza ni ya kutengeneza mbolea. Tunasema mbolea, mbolea; geological survey ipewe kazi ya kutafuta madini mbali ya natural gas, lakini kuna madini mengine kama potassium salts, kama ile ya Minjingu Phosphate, ni kazi ya madini hii.

Mheshimiwa Spika, kingine ambacho tunapaswa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa kengele ya pili imeshagonga. Ahsante sana.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Spika, haya ahsante. (Makofi)