Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii adhimu kuchangia katika Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, mabadiliko ya tabia nchi yanakwenda haraka sana. Nchi lazima iwe tayari kuchukua hatua za kukabiliana nazo. Ziko fedha nyingi duniani zinazotolewa kwenye nchi zinazozalisha hewa ya ukaa inayotokana na kutunza misitu. Nchi hii bado ina misitu mingi. Hivyo nashauri hamasa ya kutunza hii misitu na vijiji vinavyozungukwa na misitu hiyo zipewe fedha ili iwe hamasa kwao.

Mheshimiwa Spika, misitu mikubwa kama ya Kitonga na Nyang’oro mkoani Iringa ukipita wakati wa kiangazi utakuta moshi. Hii inamaanisha watu wanachoma mkaa. Hili likiendelea litaharibu zaidi mazingira na kusababisha ukame kuendelea. Serikali ione namna ya kuongeza ulinzi hata ikibidi kujenga kambi za ulinzi.

Mheshimiwa Spika, ujenzi kwenye miinuko na vilima vyote kwenye miji kama Morogoro, Iringa, Mwanza, Mbeya na kadhalika uzuiwe. Misitu hii inasaidia miji kupumua kwa maana tunapata oxygen nyingi. Binadamu na misitu tunategemeana. Wizara ione namna ya kufanya ili kuzuia kabisa kupima viwanja kwenye maeneo hayo. Nawasilisha.