Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Serikali kwa utendaji wao uliotukuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kulipa promotion za wafanyakazi, ni jambo jema, naipongeza sana Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto kubwa ninayoiona ni pale mfanyakazi anapostaafu kuna baadhi ya waajiri wanamsafirisha mfanyakazi wanapewa stahiki zao na wengine hawapewi mfano kada ya ualimu, wengine wanapewa na wengine hawapewi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ije na majibu je, stahiki hiyo ipo au imefutwa na kama ipo utaratibu wake ukoje? Nataka ufafanuzi mzuri utolewe vinginevyo nitashika shilingi. Mtumishi anapobadilisha kada anaweza kutoka kwenye mshahara wake ambao unaweza ukawa wa juu lakini kule anakoenda akashushwa mshahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli lengo la kubadilisha kada ni kutaka kupata zaidi, lakini mtu anaposhushwa kiwango cha mshahara hatuoni tuna viashiria vya rushwa na wizi katika maeneo ya kazi? Jambo hili liangaliwe namna nzuri ya kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia moja.