Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 1 Machi, 2022 kupitia barua yenye kumbukumbu namba JA.9/ 259/01A/45 lilitolewa Tangazo la kuitwa kazini kwa waombaji wa kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kati ya tarehe 29 Desemba, 4 – 29 Januari, 2022 na tarehe 7-10 Februari. Miongoni mwa kada zilizoitwa kazini ni Shirika la Reli Tanzania (TRC). Vijana 359 walishachukua barua na kupangiwa kituo cha kazi. Walipopeleka TRC HQ waliambiwa watapigiwa simu. Mpaka sasa hakuna mawasiliano yoyote, wanaomba ufafanuzi.

Pia kumekuwa na malalamiko kwa kutoka kada ya Maafisa Tarafa kwamba majukumu yameongezeka, huku mshahara umeshuka. Hivi sasa Afisa Tarafa anazidiwa mshahara na Watendaji wa Kata anaowasimamia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ufafanuzi.