Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya pembezoni kama Ukerewe yana upungufu mkubwa wa watumishi, hivyo nashauri katika ajira zinazotolewa basi maeneo haya yapewe kipaumbele. Kwa mfano, Ukerewe ina upungufu wa zaidi ya 50% ya watumishi, hivyo yaangaliwe kwa ukaribu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa watendaji wa vijiji na kata unaathiri sana shughuri za maendeleo; kwa mfano, Wilaya ya Ukerewe ina upungufu wa watendaji wa kata na vijiji 26 hali inayoathiri shughuli za maendeleo kwa wananchi. Hivyo nashauri Halmashauri zipewe haraka vibali vya kuajiri watendaji wa kata na vijiji.