Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. STELLA A. IKUPA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi wake shupavu na mahiri unaopolekea maslahi ya watumishi wa umma kuboreshwa na kuongezeka kwa ajira kwenye kada mbalimbali ambazo zilikuwa na uhaba mkubwa wa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Waziri na watendaji wa Wizara hii kwa jinsi wanavyomsadia Mheshimiwa Rais kutimiza ndoto zake kwa wananchi na ahadi zilizo ndani ya Ilani ya CCM kupitia mipango mbalimbali inayoandaliwa na Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali katika ajira zinazotolewa walau iwe inatengwa hata asilimia kati ya 10 mpaka 12 kutegemea na idadi ya ajira zilizotangazwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii.