Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. AMINA S. MOLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia Wizara hii ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Kwanza kabisa naomba niseme kwamba mimi nimekulia katika taaluma ya habari, na naomba kwa heshima na taadhima niitendee haki taaluma ya habari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Wizara husika, kwa kazi nzuri naamini kwamba atafanya mambo mazuri kadri muda unavyokwenda. Pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Ndugu Reginald Mengi, kwani yeye ndiye ambaye kwa kiasi kikubwa amechangia mimi kufika hapa, nilianzia ITV na Radio One wakati huo bado binti mdogo na baadae nikaenda Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Nichukue nafasi hii pia kumshukuru, Mkurugenzi wakati huo Ndugu Tido Dunstan Muhando, ambaye ninaamini kabisa naye amechangia mafanikio yangu hapa.
Niwashukuru pia na kuwapongeza wafanyakazi wote wa Shirika la Utangazaji Tanzania kwa kazi nzuri na ninaomba niwatie moyo, na niwaambie kwamba mwenzao nipo humu na nipo kutetea maslahi ya waandishi wote kwa ujumla na mwisho ni kwa wanahabari wote popote pale walipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo katika utangulizi wangu, basi siku zote wanasema mcheza kwao hutunzwa na mimi naomba nitunzwe kwa kuanza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kwa kuwa ndipo ambapo nimetokea huko. Shirika hili la Utangazaji Tanzania (TBC) ni shirika ambalo kusema ukweli ni kama limesahauliwa na hata ukiangalia katika bajeti ambayo imepangiwa kwa hivi sasa ni bajeti ambayo haitoshi kitu chochote; kwa mwezi mmoja tu Shirika la Utangazaji Tanzania gharama ya kulipia umeme inakwenda karibia shilingi milioni 70. Sasa kama mwezi mmoja tu na bajeti hii ambayo Shirika hili la Utangazaji (TBC) limepangiwa, utaona ni dhahiri kabisa kwamba fedha hizo hazitoshi kuweza kuikwamua (TBC) kutoka hapa ilipo ili Watanzania waweze kujivunia shirika hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yote haya na watu wamekuwa wakilalamikia ni kwa sababu Shirika hili tumelisahau, ndiyo maana kila siku linazidi kuwepo hapa lilipo. Mimi nimpongeze tu Mheshimiwa Rais kwa kutupa Mkurugenzi sasa hivi Dkt. Ayoub Rioba ambaye ninaamini kabisa ni mbobezi katika fani hii ya taaluma ya habari, ni msomi, kwa hiyo ninaamini ili aweze kufanya kazi vizuri, ni lazima haya mambo yaendane na fedha, ikiwa ni pamoja na kuboresha mitambo, kuboresha hata hayo majengo tu miundombinu katika Shirika hili imechoka tangu miaka hiyo atujazaliwa mpaka leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda Redio Tanzania pale mitambo ni hiyo, ofisi ni zile zile tangu miaka hiyo, sasa hata kama ni kijana ari ya kufanya kazi, atawezaje kufanya kazi wakati vifaa vilivyopo ni duni. Ukienda hata katika mitambo iliyopo ya Kisarawe, bado hali ni mbaya. Nashukuru kwamba kwa miaka ya hivi karibuni wameweza kuboresha angalau Redio Tanzania ambayo sasa hivi ni TBC Taifa, kidogo imeboreshwa mitambo yake, lakini hili ndilo kimbilio la Watanzania walio wengi na hasa unapozungumzia taaluma hii, hawa wa huko vijijini walitarajia mambo mengi kutoka katika Shirika hili la TBC.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali yenyewe imeisahau TBC utawezaje kuboresha? TBC ina wafanyakazi wazuri, wana taaluma lakini vifaa vimechoka. Wengine hata ofisi hawana, ukienda Shirika la Utangazaji TBC hivi sasa majengo yako pale lakini majengo hayo miunombinu hakuna chochote. Kwa hiyo, naiomba Serikali, na ninaishauri Serikali iliangalie Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa jicho la pekee, hebu tujifunze kutoka kwa wenzetu, mashirika kama CNN, BBC ambao wanajivunia hilo mashirika yao na ndiyo maana hata ukiangalia katika vita, vinapotokea vita wanachokimbilia cha kwanza ni chombo cha Taifa, kwa nini na sisi tusijivunie Shirika hili!
Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali ya Shirika hili la TBC vilevile wafanyakazi wa Shirika hili la TBC wamekuwa wakidai marupurupu na mishahara yao kwa muda mrefu. Kumekuwepo na scheme mpya ya mishahara ambayo tangu mwaka 2012 mpaka leo madai ya wafanyakazi wa TBC hayajatimizwa. Mheshimiwa Waziri Nape ninaamini kabisa haya umeshayapata na kwa sababu wewe ni kijana nakuomba uangalie kwa jicho la pekee, wasaidie hawa wafanyakazi wa TBC ili waweze kutimiza majukumu yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni Startimes, hili ni jipu! nasikitika kwa kweli. Hawa Startimes, kupitia kampuni ya Star Media ambao waliingia mkataba wa miaka mitano. Mkataba ule hivi sasa tayari muda wake umekwisha, hawa Star Media ambao ndiyo wanaimiliki kampuni hii ya Startimes, hakuna malipo yoyote yanayolipa kwa Shirika hili la TBC. Kama huu uwekezaji ulikuja na ulikuwa na nia njema, ungeweza kwa kiasi kikubwa kulisaidia shirika hili kupunguza makali, kujenga mitambo iliyopo hapo. Kwa hiyo ninamuomba Waziri atakapokuja atuambie kuhusiana na mkataba huu wa TBC, vilevile aje atueleze, kwa sababu ndani ya Star Media hawa Startimes hivi sasa wanasema kwamba wamepata hasara. Hebu tujiulize wakati tunatoka kwenye analogia kuingia kwenye digital ni nani walioongoza kwa kuuza ving‟amuzi? Nitamuomba Waziri atakapokuja atusaidie katika hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie waandishi wa habari. kila mmoja wetu hapa, hata mmoja wetu hapa asiyetegemea waandishi wa habari. Tunapokwenda popote pale msafara wa waandishi wa habari upo nyuma yetu, tukitarajia kwamba hawa ndiyo ambao waweze kufikisha taarifa kwa wananchi. Kwa nini hatuwathamini wanahabari? Kwa nini tumewasahau wanahabari? Ukiangalia hata hawa wanaofanya kazi hapa muda wote wamesimama wanafanya kazi, lakini mishahara yao ni midogo, hakuna anayewatetea.(Makofi)
Mheshimiwa Mweyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha atueleze ni lini Muswada wa Habari utakuja hapa ili tuweze kutetea maslahi ya waandishi wa habari, tuangalie pia kuhusiana na suala la bima kwa ujumla kwa hawa waandishi wa habari ili basi waweze kufanya kazi zao vizuri na ukiangalia baadhi ya wanahabari, kwa jinsi ambavyo wanatembea hata viatu vyao soli zimeisha. Kwa hiyo, mimi nina imani sana na Mheshimiwa Waziri, nina imani sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na nina imani kwamba atawatendea haki waandishi wa habari ili waweze kutimiza majukumu yao ipasavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nizungumzie suala la michezo, tunaposema michezo, michezo hii siyo tu kwa timu hizi kubwa, lakini pia hata watu wenye ulemavu wanahitaji michezo. Watu wenye ulemavu wamesahauliwa hakuna anayezungumza kwa niaba yao, kwa heshima na taadhima naomba nizungumze kwa niaba yao ili basi kilio chao kiweze kufika na Serikali iwaangalie hata kwa kuandaa viwanja ambavyo michezo hii wataweza na wao pia kushiriki na kulitangaza Taifa hili. Mwanariadha Oscar Pistorius wa Afrika Kusini, ameweza kuitangaza nchi yake ni kutokana na kuwezeshwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.