Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kupata fursa. Nami nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake, management yote ya Wizara na taasisi zake kwa kazi nzuri ambazo wanaendelea kufanya katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nita-base kwenye vitu viwili kuishauri na kutoa maoni yangu kwenye Wizara hii. Kwanza ni Chuo chetu cha Utumishi wa Umma na vile vile mafunzo kwa Watumishi wa Umma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaona kuna upokwaji mkubwa wa taasisi hii kufanya majukumu yake, kwa sababu chuo hiki kilianzishwa kwa ajili ya kuwafunda watumishi wa umma, lakini sasahivi tumekuwa na utaratibu wa kawaida kabisa kwa mtumishi kuingia ofisi ya umma pasipo kupitia kwenye chuo hiki, na ndiyo maana tunayaona haya ambayo yako kwenye mitandao. Utaona si dhambi sasahivi kuona document ya Serikali ambayo imendikwa siri kwenye Instagram, tunaona kabisa unaingia kwenye ofisi ya umma mtu amevaa kama anaenda disco, ni kawaida kabisa kwa sababu wameacha kukitumia ipasavyo Chuo cha Utumishi wa Umma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo zamani ilikuwa kwamba, ili mtumishi yeyote aanze kazi ni lazima apite kwenye chuo hiki kufanyiwa induction program. Kwenye induction program utaelezwa mipaka yako kwa nafasi yako, bosi wako umuheshimu vipi, mipaka yako inaishia wapi. Sasahivi ugomvi mwingi ulio kwenye taasisi mbalimbali ni kwa sababu watu hawapikwi kwenye chuo hiki. Mtu anaona jambo hili napaswa kufanya mimi pasipo kufanya huyu. Kwa hiyo mgongano ni mkubwa. Ni lazima Wizara ikipe msisitizo chuo hiki kuwafunda watumishi wa umma, la sivyo vitu vya kwenye mitandao na tabia za ajabuajabu za kwenye utumishi wa umma hazitakoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii kwenye hili suala la training tunaona TAMISEMI wanaajiri, wanapeleka watumishi wao Chuo cha Hombolo. Chuo cha Kodi wakiajiri wanapeleka watumishi wao chuo chao cha kodi. Wakiajiri bandari wana chuo chao cha bandari, kila taasisi zina vyuo vyao, lakini kule wakienda ukiangalia program wanazozisoma si za utumishi wa umma, wanasoma program za kama job description zao. Mfano kama bandari utakusanyaje kodi, utafanya hivi, Hombolo vilevile wanafanya hivyo. Sasa utumishi wa umma haupati fursa ya kuwafunda wale watumishi wa-behave vipi kwenye nafazi zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe coordination ndani ya Serikali. Hawa watumishi wanavyowekwa kwenye hivi vyuo; kama wakiwa Hombolo mfanye coordination mchukue chuo hiki kina wataalam wengi waende wakawape training ya utumishi wa umma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kuhusu mafunzo kwa watumishi. Ni mashahidi humu ndani ili gari hata liwe zuri ni lazima ufanye service. Unakuta mtumishi wa umma anakaa five years, haendi hata kwenye mafunzo, Kwa sasa mambo yanakwenda yanabadilika, technology zinabadilika. Ni lazima mafunzo nyawe si hiyari yawe ni lazima na wawepo na program maalum, kila baada ya muda fulani watumishi wawe wanaenda kwa kupokezana kupata mafunzo mafupi ili kuwajengea uwezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukifanya hivyo tutapunguza matatizo mengi ambayo yanawakumba watumishi wa umma na utumishi; lakini vilevile Mheshimiwa Waziri ni lazima uwe na wivu na utumishi. Utumishi wowote ndani ya nchi hii uko chini yako. Wewe ndiye unayeteuwa kwenye idara nyingine, Wizara nyingine; kwa hiyo ni lazima kuhakikisha kuna coordination ya kutosha. Hata kama TAMISEMI wanaajiri, lakini wale waishaajiriwa ni watumishi wa umma, lazima wafanye kazi kwa kufuata misingi ya utumishi wa umma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nakushukuru kwa nafasi. Naunga mkono hoja. (Makofi)